Airtel Money Yaendeleza udhamini wake katika semina ya wapiga picha wa vyombo 15 vya habari nchini


Meneja wa Airtel Money Asupya Nalingigwa (kushoto) akiongea na waandishi wa habari wapiga katika semina ya upigaji picha iliyofanyika jijini Dar Es Salaam, akifuatiwa ni Afisa uhusisano na matukio wa Airtel Dangio Kaniki na Muhadhiri wa Chuo Kikuu Richard Ndunguru.
Waandishi wa habari waliohudhuria semina ya ya upigaji picha iliyodhaminiwa na kampuni ya simu ya Airtel jijini Dar Es Salaam.

Kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel kupitia huduma yake ya kibebki ya Airtel Money kwa mara ya pili imedhamini semina ya wapiga picha wanahabari inayofanyika kwa muda wa siku mbili hapa jijini Da r Es Salaam kuanzia leo 18 hadi 19 Apili 2012.

Airtel kupitia huduma yake ya Airtel Money imedhamini kampuni ya jijini Dar es salaam ijulikanayo kama MP5 2011 entertainment kuandaa semina maalum itakayowakutanisha wataalam na wapiga picha za habari wa muda mrefu kukutana na wanahabari wapiga picha ili kubadilishana uzoefu na kujifunza mambo mbalimbali kwa lengo la kuboresha utendaji kazi zao.

Akiongea kwa niaba ya waandishi wapiga picha waliohudhuria semina hiyo Bw, Selemani Mpochi mpiga picha wa muda mrefu nchini alisema “hii ni sehemu muhimu sana kwetu wanahabari kujitengenezea utaratibu wakukaa pamoja na kutafakari mambo muhimu ili kuendelea kufanya kazi zetu kwa ufanisi,Kwa niaba ya wenzangu wote tunawashukuru sana Airtel kupitia huduma yao ya Airtel Money kwa kutudhamini katika semina hii kwa mara ya pili sasa, tunashukuru sana kwa ushirikiano wao wa kuwa tayari kutusaidia kuendeleza taaluma yetu na kuonyesha kuwa wanatambua umuhimu wa wanahabari nchini

Airtel inaendelea kuboresha huduma ya Airtel Money pesa mkononi na mpaka sasa watanzania wengi wamenufaika kwani imeweza kutoa ajira kwa watanzania wengi kupitia uwakala hivyo wananchi wengi wameweza kujipatia mapato kwa kupitia huduma hivyo semina hii ni njia nyingine itakayoweza kuinua kiwango cha mapato na uelewa wa Airtel Money kwa waandishi wa habari nchini

Zaidi ya wapiga picha za habari wapatao 15 toka vyombo vya habari nchini wanatarajiwa kuhudhuria semina hiyo jijini Dar es salaam katika ukumbi wa msimbazi center

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.