Airtel Money Yaendeleza udhamini wake katika semina ya wapiga picha wa vyombo 15 vya habari nchini
Meneja wa Airtel Money Asupya
Nalingigwa (kushoto) akiongea na waandishi wa habari wapiga katika
semina ya upigaji picha iliyofanyika jijini Dar Es Salaam, akifuatiwa ni
Afisa uhusisano na matukio wa Airtel Dangio Kaniki na Muhadhiri wa Chuo
Kikuu Richard Ndunguru.
Waandishi wa habari waliohudhuria semina ya ya upigaji picha iliyodhaminiwa na kampuni ya simu ya Airtel jijini Dar Es Salaam.
Kampuni ya simu ya mkononi ya
Airtel kupitia huduma yake ya kibebki ya Airtel Money kwa mara ya pili
imedhamini semina ya wapiga picha wanahabari inayofanyika kwa muda wa
siku mbili hapa jijini Da r Es Salaam kuanzia leo 18 hadi 19 Apili 2012.
Airtel kupitia huduma yake ya
Airtel Money imedhamini kampuni ya jijini Dar es salaam ijulikanayo
kama MP5 2011 entertainment kuandaa semina maalum itakayowakutanisha
wataalam na wapiga picha za habari wa muda mrefu kukutana na wanahabari
wapiga picha ili kubadilishana uzoefu na kujifunza mambo mbalimbali kwa
lengo la kuboresha utendaji kazi zao.
Akiongea kwa niaba ya waandishi
wapiga picha waliohudhuria semina hiyo Bw, Selemani Mpochi mpiga picha
wa muda mrefu nchini alisema “hii ni sehemu muhimu sana kwetu wanahabari
kujitengenezea utaratibu wakukaa pamoja na kutafakari mambo muhimu ili
kuendelea kufanya kazi zetu kwa ufanisi,Kwa niaba ya wenzangu wote
tunawashukuru sana Airtel kupitia huduma yao ya Airtel Money kwa
kutudhamini katika semina hii kwa mara ya pili sasa, tunashukuru sana
kwa ushirikiano wao wa kuwa tayari kutusaidia kuendeleza taaluma yetu na
kuonyesha kuwa wanatambua umuhimu wa wanahabari nchini
Airtel inaendelea kuboresha huduma
ya Airtel Money pesa mkononi na mpaka sasa watanzania wengi wamenufaika
kwani imeweza kutoa ajira kwa watanzania wengi kupitia uwakala hivyo
wananchi wengi wameweza kujipatia mapato kwa kupitia huduma hivyo semina
hii ni njia nyingine itakayoweza kuinua kiwango cha mapato na uelewa wa
Airtel Money kwa waandishi wa habari nchini
Zaidi ya wapiga picha za habari
wapatao 15 toka vyombo vya habari nchini wanatarajiwa kuhudhuria semina
hiyo jijini Dar es salaam katika ukumbi wa msimbazi center
Comments