- Get link
- Other Apps
CHELSEA YAICHAPA MAN UNITED 1-0 NA KUING'OA KOMBE LA FA
Assalaam Alaikum: Wachezaji wa Chelsea na Man United wakisalimiana
kabla ya kuanza mtanange wa marudiano ya Kombe la FA, ulioisha kwa
Chelsea kushinda kwa bao 1-0. Katika mechi ya kwanza, Chelsea ilityoka
nyuma kwa 2-0 na kupata sare ya 2-2 Old Trafford.
Na hilo je? Baada ya sare ya 0-0 lwa dakika 45 za kwanza, Demba Ba
akahiyimisha ukame wake wa mechi 10 bila kufunga bao kwa stahili!!!!
Allah Akbar; Ndivyo anavyosema Demba Ba, anayesujudu kama ishara ya
kumshukuru Mungu kwa kumjaalia kuipatia timu yake bao muhimu.
Maumivu: Beki wa kushoto wa Chelsea, Ashley Cole, akitoka kupata
matibabu baada ya kuumia katika mechi hiyo ya Kombe la FA kwenye Uwanja
wa Stamford Bridge jijini London.
Mnatisha, ila me natisha zaidi yenu: Mlinda mlango wa Chelsea, Petr
Cech akiwapa mkono washambuliaji Robin van Persie na Javier Hernandez
'Chicharito' wa Man United. Walijaribu kwa kila aina ya mikwaju, lakini
hakukubali kuruhusu bao.
No Goal: Kipa wa Chelsea, Petr Cech akipaa juu kupangua mpira wa kichwa uliopigwa na Chicharito (kulia).
Umebaaaana!!!! Chicharito akimpa mkono Cech bila kumuangalia usoni,
baada ya jitihada zake langoni kutoruhusu bao kwa dakika zot 90 za mechi
hiyo.
Hongera kwa ushindi: Wachezaji wa Chelsea wakikumbatiana kama ishara ya
kupongezana kwa ushindi wao dhidi ya Man United. Van Persie yuleeeeee -
kama hawaoni vileeeeee!!!
Comments