Taarifa kutoka kwa watu wa karibu, familia na waratibu wa dili la safari ya Mtanzania Jerry Murro na watu walioko USA walioonganisha dili ni kwamba kunako mwezi wa tisa mwaka huu kijana ataweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza na mwanaeast afrika wa kwanza kukalia kiti cha studio za shirika kubwa la utangazaji duniani la Cable News Network (CNN) lililo na makao yake makuu jijini Atlanta jimbo la Georgia nchini Marekani. Waratibu wa dili hilo wanasema Jerry alipigiwa pande na Profesa mmoja katika chuo kikuu kimoja kilichopo jimboni Georgia aitwaye Rachel Copper, prof huyu alivutiwa na dvd za kazi za jerry muro na hatimaye kijana akaitwa kwa usaili na fununu ni kwamba kijana alipita katka interview. Inasemekana kijana atakuwa anauza nyago katka vipindi vya utafiti na documentaries mbalimbali ztakazokuwa znaruka hewani na CNN na hata pia kwenye LIVE COVERAGES atakuwa akionekana katika viti vya studio hizo jijini atlanta ambazo zipo karibu na zile studio kubwa ya uzalishaji music ATLANTIC RECORDS.
Chanzo JF
Kwa kuwa tunaye humu tunaweza pata lolote toka kwake.
Comments