Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye
akizungumza na waandishi wa habari leo Aprili 4, 2013, katika Ukumbi wa
Sekretarieti, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es
Salaam. Picha na Bashir Nkromo
--
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi,
Nape Nnauye ameishukia Chadema na kudai kwamba viongozi wa Chama hicho
wanatumiwa na baadhi ya mafisadi kujaribu kumchafua Waziri wa Uchukuzi,
Dk. Harrison Mwakyembe.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Aprili 4,
2013, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Dar es Salaam, Nape
amesema, hatua ya mmoja wa viongozi wa ngazi ya juu wa Chadema kutoa
tuhuma dhidi ya CCM kuwa kupitia kampuni yake ya Jitegemee Trading,
imeingia mkataba na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) katika mradi wa
upanuzi wa Bandari Kavu kwa kutumia eneo la SUKITA lililopopia ni uzushi
ambao Chadema wamelishwa na mafisadi hao.
Nape alisema tuhuma hizo ambazo zimechapishwa leo
Aprili 4, 2013, na baadhi ya vyombo vya habari hasa Tanzania Daima
zikidai Chadema wameibua unaoitwa ufisadi wa Mwakyembe wa kuipa CCM
zabuni ya kupanua bandari si za kweli.
Amesema uongo huo Chadema wamelishwa na baadhi ya
mafisadi waliotaka kutumia eneo hilo la CCM kujaribu kukaa katikati ya
mwekezaji yeyote atakayejitokeza na Jitegemee kwa lengo la kujinufaisha
wao binafsi na kwamba hatua hiyo ni mwendelezo wa Chadema kutumiwa na
mafisadi katika kutimiza mambo yao na kutumika huko kunasukumwa na kiu
ya Chama hicho kutaka kushika dola kwa gharama yoyote.
Nape alisema kibaya zaidi katika tuhuma hizo,
Kiongozi huyo wa Chadema alikwenda mbali kwa kuishutumu Wizara ya
Uchukuzi na Waziri wake Dk. Harrison Mwakyembe kwa madai ya kukiuka
taratibu na kutoa zabuni ya upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam kwa CCM
tena kinyume na taratibu za manunuzi.
"Ukweli ni kwamba Kampuni ya Jitegemee Trading
Company ni mali ya CCM, na pia ni kweli kuwa kiwanja kilichotajwa ni
mali ya CCM kilichokombolewa kutoka zilizokuwa mali za SUKITA ambayo pia
ilikuwa kampuni ya CCM, lakini TPA na Jitegemee mpaka sasa hawajaingia
mkataba wowote.
Alisema ukweli ni kwamba eneo hilo limeombwa na
wawekezaji wengi wakiwemo TPA na masharti waliyopewa wote ni kuwasilisha
mapendekezo ya mipango yao ya kibiashara kabla ya kufikiriwa uamuzi wa
nani awekeze kwa ubia na Jitegemee kwenye eneo hilo.
"Wanachokiita wenzetu wa Chadema kuwa ati ni zabuni
iliyotolewa kwa kampuni ya Jitegemee na Mamlaka ya Bandari ni barua ya
TPA kwenda Jitegemee wakiomba ridhaa ya kushirikiana kuliendeleza eneo
la kampuni hiyo ya Jitegemee lenye ukubwa wa zaidi ya ekta 100, katika
mfumo wa ushirikiano yaani "Joint Venture" kupitia utaratibu wa PPP
(Public, Private Partnership) jambo ambalo ni la kawaida sana kwani
linafuata utaratibu na sheria zote husika", Nape alifafanua.
Alisema, Chama Cha Mapinduzi kinamiliki Kampuni ya
Jitegemee, na kwamba pamoja na umiliki huo, kampuni hiyo imekuwa
ikitekeleza shughuli za uwekezaji kwa muda mrefu kwa kufuata taratibu
zote na sheria za nchi kwa ujumla.
"Tunatambua kuwa Chadema kwasasa wanapitia wakati
mgumu sana kisiasa kutokana na kuanza kuvuna walichopanda kwa muda mrefu
katika siasa za nchi yetu. Lakini pia tunatambua tabia ya viongozi wa
Chama hicho ya kudandia kila gari linalopita bila kujua linakokwenda kwa
kugeuza kila kinachofanyika nchini, ilimradi hakifanywi na wao basi ni
haramu", alisema Nape na kuongeza;
"Hata hivyo mazingira hayo wanayopitia Chadema
hayawapi uhalali wa kuwa wavivu wa kufikiri kiasi cha kushindwa
kutofautisha barua ya maombi ya kushirikiana kuendeleza eneo na mkataba,
aidha mazingira wanayopitia kwa sasa hayawapi uhalali wa kuwa wavivu wa
kufikiri kiasi cha kushindwa kujua kuwa kinachofanyika ni mawasiliano
ya awali sana ya kusudio la kuendeleza eneo husika na hakuna taratibu
zilizokiukwa".
Nape alidai umbumbumbu wa aina hiyo unatia mashaka
sana juu ya uwezo wa Chadema wa kufikiri na kupambanua mambo na kwamba
jambo moja wanaloonekana kulimudu ni uwezo wao wa kutunga uongo na
kupanga machafuko. "Na hii ndio siri ya watanzania kuwakataa kila
kukicha na ndio siri ya kufa kwa chama hicho, kwani njia ya muongo ni
fupi", alisema Nape.
"CCM inachukua nafasi hii kuipongeza Wizara ya
Uchukuzi kwa kazi nzuri inayoendelea kuifanya chini ya Dr. Harrison
Mwakyembe hasa ya kuongeza ufanisi kwenye bandari yetu ya Dar es salaam.
Tunawataka wasikatishwe tamaa na mafisadi wachache, wachape kazi kwa
uzalendo huohuo waliouonesha
Comments