Kinana amaliza ziara yake morogoro vijijini,akagua miradi mbalimbali ya maendeleo.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Meneja Mradi wa mashamba ya Mfano ndani ya kijiji cha Pangawe,wilaya ya Morogoro vijijini,Bwa.Kim Sun Ho wa KOICA walipokuwa wakitembelea Shamba hilo lenye Wakaazi  wapatao 180,ambao wanasimamiwa na kupewa mafunzo ya Kilimo cha kisasa na ufugaji bora kutoka kwa shirika la Maendeleo la Korea (KOICA).

Kinana na Ujumbe wake wa chama hicho walitembelea mradi huo katika ziara yao ya kichama,Wakaazi hao wanamiliki zaidi ya hekari 150 kila mmoja ana magunia  nane ya mahindi waliyovuna mwaka jana huku wakiwa na na kiasi cha shilingi milioni 50 benki.CCM imefanya  ziara katika Wilaya ya Morogoro vijijini na kufungua mashina na matawi ya chama hicho huku akipokea wanachama wapya waliojiunga na waliotoka vyma vya upinzani.
 Sehemu ya Shamba la mfano la Mahindi.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo mafupi kutoka kwa Meneja Mradi wa KOICA,Bwa.Kim Sun Ho wa KOICA,alipotembelea mradi wa majengo yatakayotumika katika mafunzo ya ufugaji wa kisasa katika kijiji cha Pangawe,Wilaya ya Morogoro Vijijini.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akijadili jambo na Katibu wa NEC Itikadi Siasa na Uenezi CCM,Nape Nnauye walipotembelea mradi wa majengo yatakayotumika katika mafunzo ya ufugaji wa kisasa katika kijiji cha Pangawe,Wilaya ya Morogoro Vijijini.

Pichani ni Sehemu ya soko la Kisasa la Mkuyuni linalojengwa na CCM kwa gharama ya shilingi milioni 100,katika kata ya Mkuyuni,ndani ya Morogoro Vijijini.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdurlhaman Kinana akiangalia kazi za ujasiliamali zinazofanywa na mkazi wa kijiji cha Makuyuni,Mkaazi huyo ameamua kujiajiri kuwa kutengeneza mafagio ya njiti na kuyauza kwa wananchi wa eneo hilo,kwa ajili ya kujiongezea kipato.
 Ndugu Kinana na ujumbe wake wa CCM wakielekea kukagua ujenzi unaoendelea wa kituo cha afya (zahanati) ya  Mkuyuni.
 Ujenzi wa jengo la kituo cha zahanati ya Mkuyuni ukiendelea  . 
 Mmoja wa Wahudumu wa kituo cha afya cha Mtamba-Matombo wilaya ya Morogoro Vijijini, kilichopandishwa hadhi na kuwa Zahanati,Bi.Lilian Peter Haule akitoa maelezo mafupi ya maendeleo ya upanuzi wa ujenzi wa  zahanati hiyo ya Mtamba kwa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdurlhaman Kinana.
 Ndugu Kinana akikamkabidhi kadi mpya,katibu kata wa Kiroka kutoka chama cha CUF,Hadim Omary,Wilaya ya Morogoro Vijijini.
Mwenyekiti wa CHADEMA kata ya Kiroka akikabidhi kadi na bendera ya chama hicho kwa Ndugu Kinana,na kuwapokea kama wananchama wapya wa chama cha CCM na kuwakabidhi kadi mpya.




 Wakazi wa Kata ya Kiroka,wakishngilia jambo walipokuwa wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman alipozungumza nao mara baada ya kuzindua jiwe na la msingi la ofisi hiyo. 
 Katibu tawi la Gumba kutoka chama cha CUF,Said Almas akirejesha kadi yake ya na kupokea kadi mpya ya CCM,akijiunga kuwa mwananchama mpya kutoka kwa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrhman Kinana.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdurlhaman Kinana akipewa zana za kimila kutoka kwa Chifu Kingaru wa kabila la Waruguru .
  Wananchi wa Kata ya Mvuha-Matombo wakimsikiliza Katibu wa NEC Itikadi Siasa na Uenezi wa CCM Nape Nnauye,aidha Ndugu Kinana na ujumbe wa CCM umehitimisha ziara yake ya Morogoro vijijini na leo wataunguruma Morogoro mjini ikiwemo pia kukagua  maendeleo ya miradi ya mbalimbali ya chama hicho ikiwemo na kukiimarisha chama.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA