KLABU YA SIMBA YAMPONGEZA HANS POPPE KWA KUREJEA SIMBA
MWENYEKITI wa Simba, Mhe, Ismail Aden Rage, amemshukuru
aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu, Zacharia Hans Poppe, kwa
kukubali kurejea kushikilia nyadhifa zake zote.
Poppe alitangaza kujiuzulu nyadhifa zake za uongozi ndani ya
Simba Machi 7 mwaka huu, kutokana na hali ya migogoro iliyokuwapo wakati huo.
Hata hivyo, Rage alikataa kujiuzulu huko kwa Poppe na
akasema atamshawishi abadili maamuzi kwa manufaa ya Simba.
“Napenda kutumia nafasi hii kuwaarifu wana Simba popote
walipo kwamba Poppe amerejea na yuko tayari kuitumikia Simba kama
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba,”
alisema Rage.
Kwa upande wake, Poppe alisema amerejea Simba kutokana na
utulivu ulioanza kujitokeza klabuni na kwamba nia yake ni kuhakikisha klabu
inafanya usajili mzuri na wa kiwango kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu.
Imetolewa na
Ezekiel Kamwaga
Ofisa Habari
Simba SC
Comments