Makinda 'amewatusi' Waandishi?
Na Bryceson Mathias
APRILI
29, 2013 akiwa Mbeya, Waziri Wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa Bernard Membe, alikerwa na tabia ya baadhi ya
Wasomi Wanaotumia Elimu yao kuikana Nchi yao, ambapo wamefika mahali
wanaipuuza na kuonesha ubinafsi wa kuwashawishi wafadhiri wainyime
misaada Tanzania.
Tabia hiyo nimeifananisha
na kauli iliyotolewa na Spika wa Bunge Anne Makinda aliyoitoa bungeni
akijibu mwongozo wa Mbunge wa Ubongo John Mnyika (Chadema), ambapo
aliwapuuza Waandishi wa Magezetii na vyombo vyao kuwa, hafanyi kazi na
vyombo vya habari kwa kwa sababu yanaandika habari za Uongo.
Pengine
haikuwa vizuri kwa Makinda, kuvijumuisha Vyombo (Magazeti) na Waandishi
wote, Iwapo Chombo kimoja au Mwandishi Mmoja aliwahi kuandika Uongo,
kama ambavyo baadhi ya Wabunge kwa makusudi yao waliamua kutoa Matusi ya
Nguoni bungeni, ila wandishi hawakusema Bunge limetukana.
Magazeti
hayo hayo ambayo Spika anayaita yanaandika Uongo, ndiyo yaliyomnadi
akiomba Ubunge, Uspikana hata sasa akiendesha Bunge yamekuwa yakiendelea
kumnadi. Je, kila kinachoandikwa akiendesha Bunge, Hotuba anazotoa
ndani na nje ya Bunge ni za Uongo?
Kama
ni za Uongo mbona Spika Makinda, hata siku moja hajawahi kukinyoshea
Chombo, Habari, na Mwandishi anayedhani aliandika Uongo ili asutwe kwa
taratibu na miongozo na sheria za Kihabari, kuainisha Kero yake hiyo?
Ni
wazi Makinda anafahamu vipo vyombo mahususi vya kutatua Migogoro,
Malalamiko na Mafanikio ya Habari na Changamoto zake, likiwemo Baraza la
Habari Tanzania (MCT), Umoja wa Vyama vya Habari Tanzania (UTPC), Vyama
vya Wandishi vya Mikoa, na Wamiliki wa Vyombo vya Habari (MOAT).
Hivyo,
kimsingi kuwararua Wandishi wote bila kutenga Chombo, Mwandishi au
habari husika, ni fedheha ya kuwapuuza wandishi wa nchini ambao kimsingi
pamoja na mapungufu wamefanya kazi nzuri mno, kuwanandi, wabunge
wenyewe akiwemo Makinda na wananchi na uchumi wao.
Kitendo
hicho kimewatangza vibaya wandishi wa Tanzania Kitaifa na Kimataifa,
Jambo ambalo pasipo kufahamu linaaaweza kuathiri biashara ya Magazeti na
Heshima ya Wandishi kwa ujumala wao, wanapokuwa kwenye majukumu yao.
Je,
Wandishi ambao wametajwa bungeni kuwa wanaandika habari za Uongo wakiwa
hawapo humo, wakikusudia kugomea kuandika Shughuliza zozote
atakazofanya Spika Anne Makinda na Ofisi yake, kama walivyowahi
kufanyiwa Mawaziri kadhaa hadi afute Kauli, atajisikia vizuri?
Sikatai
hakuna habari zinatia shaka, La Hasha! Habari hizo zipo, na wandishi
wanaweza kuwa wapo, na cha ajabu unaweza kukuta vyombo vya Chama Tawala
na Serikali ndiyo vinavyoongoza kupotoa habari, vikifuatiwa na vya
binafsi. Je amewahi kuvinyoshea kidole?
Udhaifu
kwa kila upande upo sikatai, na naamini mkulima hawezi kulima bila
kujikata. Lakini ni vema kuelezana katika wema, badala ya kukurupuka na
kusema maeneo kwa Jazba ambayo inabomoa murua na misingi ya mustakabali
wa Kazi na Biashara tunayoitegemea.
Aidha
Hata Kiti cha Spika, si kwamba maamuzi yake yote kinayofanya kwenye
Kiti ni Sahihi! Mengine yanaonekana wazi kabisa pale mtu Kateleza, hadi
wananchi wanaosikia wanasema Haaaaaaaaaaaaaaa kama anavyokosa mchezaji
kufunga Goli!
Mfano, pia Kiti kama wandishi kina makosa yanayotumiwa katika utaratibu
unaotumika sasa wa kura za ndiyo na hapana ni wa zamani na hautendi
haki, kwani huegemea zaidi uamuzi wa Spika na si wabunge. Upitishaji hoja kwa kupiga kura na “Waliosema Ndiyooo wameshinda” haufai Bungeni!
0715933308
Comments