MAMA SALMA KIKWETE APEWA NISHANI YA KAZI ZA WAMA KUTOKA TAASISI ILIYOPO LONDON, UINGEREZA
Mh. Naibu Spika Job Ndugai akipokea Nishani hiyo kutoka kwa Dr. Mohammed Zaharani . Wakiangalia kwa furaha ni Mh. Beatrice Shelukindo, Bi Mariam Mungula na Nd. Haruna Mbeyu. |
Baadhi
ya Akina Mama waKitanzania waliohudhuria hafla hiyo katika picha ya
upendeleo na M. Beatrice Shelukindo na Nishati ya Mama Salma.
|
Mke
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambae pia ni Mwanaharakati
wa Kijamii kupitia Chama Chake cha Wanawake na Maendeleleo, wiki
iliyopita alizawadiwa Nishani na Chama kinachojishughulisha na kuinua
kiwango cha Elimu kwa Nchi za Afrika Mashariki kilichoko katika jiji la
London, Uingereza.
Akiongea
katika Hafla hiyo fupi iliyofanyikia katika kumbi za Hoteli ya Park
Plaza iliyopo pembeni mwa Westminster Bridge (katikati ya jiji la
London) Dr Mohammed Zaharan ambae ni Katibu wa Chama hicho cha East
Africa Education Foundation (EAEF) alisema kuwa Chama Chake kimekuwa
kikifuatilia kwa ukaribu na shughuli zinazofanywa na Mama Kikwete
kupitia Jumuiya ya WAMA na wamefurahi kupata
fursa
hii ya kumtunukia "Award" kwa mchango wake mkubwa sana wa kuinua Elimu
ya Mtoto, hususan wa kike na vilevile kuwezesha Wanawake ili waweze
kujitegemea. Dr Zaharani aliongeza kuwa Mama Kikwete ni mfano bora sana
wa kuigwa na Wanawake katika jamii ndani na nje ya Tanzania.
Akipokea
Nishani hiyo kwa Niaba ya Mama Salma Kikwete, Naibu Spika Mh. Job
Ndugai (Ambae alikuwa Nchini Uingereza kwa Mualiko wa Naibu Spika wa
Uingereza na aliongoza na Wabunge ambao ni Wajumbe wa Kamati ya Utumishi
ya Bunge) alisema kuwa amefurahishwa sana na kitendo hicho cha Mchango
wa Mama Salma kuonekana, kwa kuwa kinadhihirisha mchango unaofanywa na
Jumuiya zisizo za Kiserikali katika jamii kama WAMA unaonekana mpaka Nje
ya Tanzania.
Nae
Mh. Mama Beatrice Shelukindo alifurahi zaidi kwa kitendo hiki na kusema
kuwa hili ni jambo kubwa sana na linadhihirisha mchango mkubwa wa Mama
Salma katika kumuendeleza Mwanamke wa KiTanzania na inatoa moyo kwa
Wanawake Wengine.
HONGERA
SANA MAMA SALMA NA MWENYEZI MUNGU AZIDI KUKUONGOZA NA KUKUPA AFYA NJEMA
ILI UWEZE KUCHANGIA ZAIDI KATIKA MAENDELEO YA MWANAMKE NA MTOTO WA
KIKE.
Comments