Mkuu wa Jeshi la Magereza
nchini, Kamishna Jenerali John Minja (kulia), akikata
utepe kuzindua rasmi jukumu la kuwasafirisha Mahabusu kutoka Gerezani
kwenda Mahakamani na kurudi Gerezani kwa Mkoa wa Dodoma. Katikati ni
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, Mary Shangali, kushoto
ni Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP), Dk.Eliezer Feleshi ambao walikuwa
katika uzinduzi huo uliofanyika katika Gereza Kuu Isanga Dodoma.
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, Kamishna Jenerali
John Minja, akiwasha moja ya magari yaliyozinduliwa kuashiria uzinduzi
wa kuwasafirishia Mahabusu kutoka Gerezani kwenda Mahakamani na kurudi
Gerezani kwa Mkoa wa Dodoma. Uzinduzi huo ulifanyika katika Gereza Kuu
Isanga Dodoma.
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, Kamishna Jenerali
John Minja akitoa hotuba yake kabla ya kuzindua mabasi mawili na gari
ndogo moja (pick-up) kwa ajili ya kuwasafirishia mahabusu toka gerezani
kwenda mahakamani na kurudi gerezani kwa Mkoa wa Dodoma. Katika hotuba
yake mkuu wa jeshi hilo aliwataka maofisa magereza wa mkoa huo wawe
makini kuyatunza magari hayo. Uzinduzi huo ulifanyika katika Gereza
Kuu Dodoma.
Mkuu wa Jeshi la Magereza
nchini, Kamishna Jenerali John Minja (kushoto) akisalimiana na
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, Mary Shangali baada ya
uzinduzi wa mabasi mawili na gari ndogo moja (pick-up). Kushoto
Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP), Dk.Eliezer Feleshi. Uzinduzi huo
ulifanyika katika Gereza Kuu Dodoma.
Magari matatu ya kuwasafirisha Mahabusu yaliyozinduliwa
na Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, Kamishna Jenerali John Minja, katika
hafla iliyofanyika Gereza Kuu Isanga Dodoma.
PICHA ZOTE NA KITENGO CHA MAWASILIANO
YA SERIKALI
WIZARA
YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.
Comments