WAKULIMA WAKISHITAKI KIWANDA CHA MTIBWA KWA CCM


*Wakulima waorodhesha madhambi ya kiwanda
*Wamhusisha Mkapa kukimiliki, Kinana ataka suluhu

Na Mwandishi Wetu, Mvomero

WANANCHI wa Wilaya ya Mvomero  mkoani Morogoro wamekishtaki Kiwanda cha Sukari Mtibwa kuwa kimekuwa kikifanya dhuluma kubwa zidi ya wakulima wa miwa huku wakimuomba Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), kufanya kila analoweza kuhakikisha mgogoro uliopo kati ya pande hizo mbili unapatiwa ufumbuzi.

Pia wamesema kwa hali iliyofikia imefanya wananchi wa Wilaya ya Mvemero kutokuwa na imani na Serikali na katika hilo wanaomba pia CCM kufanya kila linalowezekana kutafuta ufumbuzi ili wananchi hao warudishe matumani kwa chama hicho ambacho bado kinakubalika kwa Watanzania wengi.

Wakati hayo yakiendelea, uongozi wa Kiwanda cha Sukari Mtibwa umeweka wazi kuwa kinatambua baadhi ya changamoto zilizopo baina yao na wakulima na kwamba sasa ni wakati wa kutafuta ufumbuzi wake na kuanza ukurasa mpya lakini pia wakaomba CCM kuiomba Serikali kuangalia wawekezaji wa ndani kwani kuna sukari inayotokana nje na kufanya wakose fedha.

Wakizungumza wilayani hapa jana wakulima wa miwa na wawakilishi wao walimambia Kinana aliyeambatana na viongozi wa ngazi mbalimbali wa chama hicho akiwemo Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye, walisema mgogoro umedumu kwa miaka 10 lakini kwa bahati mbaya hakuna majibu ya suluhu hali inayofanya wananchi wajiulize maswali bila majibu.

Walisema kuwa yapo mambo mengi ambayo hawafuri kuona yakifanywa na wawekezaji wa kiwanda hicho kwani badala ya kuwa na manufaa kwao sasa kimekuwa mateso ambayo sasa yanahitaji ufumbuzi wa kudumu.

Walitaja baadhi ya matatizo makubwa yanayofanywa na kiwanda cha Mtibwa ni kucheleweshwa kwa malipo ya miwa, kiwango kidogo cha malipo pindi wanapopeleka mazao yao kuuza kiwandani, madeni sugu kwa wasataafu wa kiwanda lakini kubwa zaidi wanadai kuna dhuluma ambayo imekuwa ikifanywa na uongozi wa kiwanda hicho.

Akizungumza wakati akieleza matatizo wanayokumbana nao wakulima wa miwa, mmoja wa wawakilishi wa wakulima hao, Alfan Mbila alisema wakulima wamekata taa kutokana na vitendo vinavyofanywa na kiwanda hicho.

“Wakulima hawalipwi kwa wakati, wastaafu nao hawalipwi mafao yao na hata wakienda mahakamani wanashangaa wanashindwa kesi na mwekezaji kuibuka mshindi hata katika kesi zao za msingi za madai.

“Tumefika mahali sasa wakulima tunajiuliza maswali mengi, hivi kiwanda hiki ni cha nani?Maana haiwezekani uongozi wa kiwanda cha Mtibwa kuwa na nguvu kubwa kuliko Serikali.Umekuja Kinana na Nape tunaamini hili mtalimaliza na kupata ufumbuzi wa kudumu.Tumechoka na inafaka mahali tunaona ni bora tukapewa kibali tuanze kiwanda chetu cha kusindika miwa ili tuachane na Mtibwa,”alisema.

Wananchi hao ambao waliamua kutumia mkutano huo kukishtaki kiwanda hicho na kukitaka chama hicho kuchukua hatua zaidi walikwenda mbali na kudai huenda kata ya Turiani imekwenda upinzani kwasababu ya wananchi kutofurahishwa na mwenendo na matendo  ya kiwanda hicho na matokeo yake kuichukia Serikali.

Mkulima mwingine Ramadhan Mhuta alisema kuwa matatizo mengine kati yao na kiwanda cha Mtibwa yalianza tangu mwaka 1998 baada ya kupewa kiwanda hicho kutoka kwa Serikali na tangu wakati huo yameibuka mambo mengi ambayo yamefanya mgogoro kuwa mkubwa na kuonekana kama umekosa ufumbuzi wake.

“Tunaomba Kinana hili uchukue kama changamoto ambayo inahitaji majibu yatakayomaliza tofauti zilizopo.Imefika mahali wananchi wanachukua wawekezaji hao.Wapo wengine wanaamini kiwanda hiki ni mali ya Rais Mstaafu Benjamin Mkapa.Hivyo pamoja na majibu mtakayotoa, tunataka kufahamu hiki kiwanda ni mali ya nani?Alihoji Mhuta.

 Mwakilishi wa wakulima wa kata ya Kanga, Mohamed Hamis alisema kuwa tatizo lililopo si mwekezaji bali ni matendo yake ambayo yanaonekana ni dhuluma dhidi ya wakulima.

Alisema kinachotakiwa Kinana anatakiwa kutafuta ufumbuzi ambao utaondoa migogoro iliyopo na si vinginevyo huku akiweka wazi kuwa hata Nape akiamua kuwa mwekezaji si tatizo bali matendo yake kama hatafurahisha wananchi hilo ndilo litakuwa tatizo.

Akijibu baadhi ya tuhuma zilizoelekezwa dhidi ya kiwanda hicho, Mwakilishi wa Kiwanda cha sukari Mtibwa, Hamad Yahya Juma alisema alisema madai yaliyotolewa na wananchi si ya kweli na kwamba wamekuwa wakijitahidi kadri wanavyoweza kutenda haki.

Aliongeza kuwa waatambua kuna baadhi ya changamoto zilizopo zikiwemo za kutolipa baadhi ya michango ya PFF lakini kwani  wakati lakini kwa ujumla wanalipa.

Kuhusu madai ya wastaafu kutolipwa, alisema Mtibwa haidai na wastaafu ila kinachotokea kuna madeni ya kurithi ambayo yalitokana na Serikali huko nyuma kutolipa lakini kwa uungwana wa kiwanda chao uliamua kurithi deni na kwa kiwango kikubwa wamefanikiwa kulipa.

Akizungumzia suala la dhulma wakati wa uvunaji miwa shambani, alisema hiyo si kweli kwani ni miaka mitatu sasa miwa inavunwa na wakulima wenyewe kupitia vyama vyao vya ushirika, inapofika mahali wakulima wanatoa lawama kwa kiwanda si kutenda haki na katika hilo aliwataka wawe wakweli mbele ya Kinana.

Wakati hayo yakiendelea, Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mvomero , Jonas Van Zeland alitumia nafasi hiyo kuwambia Kinana kuwa wanakidai kiwanda sh.milioni 280 ambazo zinatokana na makato ya wakulima ambazo zinatakiwa kwenda kwenye halmashauri.

Akijibu hoja hizo wakati akifanya majumuisho, Kinana alisema yapo mambo nane ya msingi ambayo yametolewa na wakulima hao lakini hataki kuingia kwenye mkumbo wa ahadi ambazo hazitekelezeki na kwa hali hiyo ameamua kukutana tena na wawakilishi wa pande zote ili kuzungumzia kwa kina na kupata ufumbuzi wa kudumu.

“Hili si la kutoa majibu ya haraka, nipeni muda na mimi nifahamu.Naomba wawakilishi wa makundi yote pamoja na uongozi wa kiwanda Jumatatu tukutane Morogoro.Ziara yangu inakwisha Jumapili lakini sitaondoka hadi tukae tuzungumze.

“Kwa hali ilipofikia sasa, ukionekana tu unapita pita huku Mtibwa unaonekana na wewe unahusika na kiwanda hicho.Wengine wanaamua kusingizia kiwanda hiki ni mali ya kigogo wakati mwingine anatajwa mzee Mkapa.

“Masikini huku ni kusingizia, lakini hayo yote yanatokana na kuwepo kwa matatizo yaliyokosa majibu.Kama hakukuwa na matatizo wakulima wanalipwa vizuri na kila kitu kinakwenda sawa usingesikia kiwanda kinamilikiwa na nani.Kama kuna dhuluma ndio hayo yote yanaibuka,”alisema Kinana.

Alitoa angalizo kuwa, CCM haishughulikii mgogoro huo kwasababu ya kutafuta kura maana hiyo si hoja, bali inafanya hivyo kwa kuwa tumekabidhiwa dhamana na Watanzania ya kuliongoza taifa hili na kutafuta ufumbuzi wa matatizo yao.

“Hivyo kinachofanyika hapa, ni kazi yetu sisi CCM kama chama tawala.Tukianza kuingiza mambo ya kukosa au kupata kura kwa sasa hayana maana.Tukitafuta ufumbuzi wa matatizo wananchi watapima wenyewe na si kuangalia kura zao,”alisema Kinana.
Mwisho

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*