WATU MILIONI 14 WANUFAIKA NA HUDUMA YA MATIBABU YA MABUSHA NA MATENDE TANZANA: DK. MWELE.


Na Mroki Mroki wa Father Kidevu Blog Arusha
Wilaya 94 zimefikiwa katika zoezi la unyweshaji dawa za Matende na Mabusha  na utoaji elimu linaloendeshwa chini ya Mpango wa Taifa wa Kudhibiti magonjwa yasiyopea kipaumbele (NTD) unaoratibiwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.

Mkurugenzi Mkuu wa NIMR Dakta Mwelecele Malecela ameyasema hayo mjini Arusha wakati akizungumza na waandishi wa Habari katika Kongamano la 27 la taasisi hiyo la  Sayansi la Kongamano la Pili la Afya Moja Afrika  linaloendelea mjini humo.

Dk. Malecela amesema watu milioni 14 wamenufaika na huduma ya matibabu ya mabusha na matende  katika wilaya hizo 94 ambazo zimefikiwa katika zoezi la ugawaji dawa na tiba.

Aidha alieleza kuwa katika wilaya ya pangani jumla ya watu mia mbili waliokuwa wanasumbuliwa na mabusha wamepatiwa tiba kwa
njia ya upasuaji na tayari wamerejea katika hali ya kawaida na kuweza kuendelea na shughuli za maendeleo ya jamii yao.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU