XAVI AVUNJA REKODI YA PASI ULAYA, AWAFUNIKA WOTE UNAOWAJUA


HAKIKUWA kiwango bora kilichoonyeshwa na Barcelona, lakini kwa Xavi ulikuwa ni usiku mzuri wa kuukumbuka: akipatia kwa asilimia 100 katika pasi zake zote 96 alizopiga dhidi ya Paris St Germain jana.  
Vigogo hao wa Catalan walitolewa jasho kupata nafasi ya kutinga Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa, walipokuwa nyuma kwa bao 1-0 ndani ya dakika ya 50 na hatimaye kufuzu tu kwa faida ya mabao ya ugenini, baada ya Pedro kusawazisha dakika ya 71. 
Unblemished record: Xavi found an team-mate with every pass against Paris St Germain
Rekodi: Xavi alimfikishia kila pasi kila mchezaji mwenzake aliyempelekea jana dhidi ya Paris St Germain
Unblemished record: Xavi found an team-mate with every pass against Paris St Germain
Wengi watasifia kuingia kwa Lionel Messi katikati ya kipindi cha pili kama siri ya mafanikio ya Barca jana, lakini alikuwa ni Xavi aliyecheza kwa ubora wa hali ya juu katika nafasi ya kiungo. 
All smiles: Xavi savours success at the Nou Camp with team-mate Andres Iniesta
Tabasamu: Xavi akifurahia kwenye Uwanja wa Nou Camp jana na mchezaji mwenzake Andres Iniesta
Mspanyola huyo mwenye umri wa miaka, 33, alikaribia kufunga dakika ya kwanza tu baada ya shuti lake la mpira wa ashabu kudondokea nyuma ya nyavu na wengi uwanjani kudhani ni bao.  
Alicheza dakika zote 90 katika mechi hiyo na alifanikiwa kumfikishia pasi kila mchezaji mwenzake aliyempelekea na kuwapiku wachezaji wengine wote kwa miaka 10.
Kazi nzuri ya Xavi jana kwa asilimia 100 anawapiku Javier Zanetti dhidi ya Tottenham miaka mitatu iliyopita na nyota wa zamani wa Arsenal, Emmanuel Eboue anayeshika nafasi ya tatu katika orodha. 
Lakini wakati Mspanyola huyo anamudu kupiga pasi zake kwa asilimia 100, Zanetti na Eboue walipiga kwa usahihi pasi 72 na 54 katika mechi zao.   
Inafahamika uwezo wa Cristiano Ronaldo unamfanya awepo katika orodha, lakini hamuachi mbali Nahodha wa Chelsea, John Terry aliyefanya kazi nzuri dhidi ya Werder Bremen kwenye michuano hiyo mwaka 2008.
Catch him if you can: Xavi was instrumental in Barca's progress into the semi-finals of the Champions League
Mkamate kama unaweza: Xavi alikuwa kila kitu Barca ikifuzu Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa jana
Catch him if you can: Xavi was instrumental in Barca's progress into the semi-finals of the Champions League

WAKALI WA PASI MURUWA LIGI YA MABINGWA TANGU MSIMU WA 2003/04 

MECHIMWAKAMCHEZAJIIDADI YA PASI
Barcelona v PSG2013Xavi96
Inter vs Tottenham2010Javier Zanetti72
FC Porto vs Arsenal2006Emmanuel Eboue54
Barcelona vs Stuttgart2007Lilian Thuram50
Real Madrid vs Man City2012Cristiano Ronaldo50
Braga vs Galatasaray2012Paulo Vinicius 48
Basel vs Barcelona2006Martin Caceres48
Chelsea vs Werder Bremen2008John Terry47
FC Porto vs Dynamo Kiev2006Rolando45
Roma vs Real Madrid2004Ivan Helguera43
Real Madrid vs Dinamo Zagreb2011Sergio Ramos43

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI