Abwao, Lukuvi walipuana
Dodoma.
Mbunge wa Viti Maalum (Chadema) Iringa, Chiku Abwao na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi jana waligeuza Bunge kama jukwaa la kufanyia kampeni za kuwania ubunge kwa jimbo la Isimani kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.
Mbunge wa Viti Maalum (Chadema) Iringa, Chiku Abwao na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi jana waligeuza Bunge kama jukwaa la kufanyia kampeni za kuwania ubunge kwa jimbo la Isimani kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.
Hali hiyo ilifanya Spika wa Bunge, Anne Makinda
kuingilia wakati Abwao akizungumza na kumtaka arudi kwenye hoja,badala
ya kumshambulia Lukuvi na kupiga kampeni, lakini Mbunge huyo alishikilia
kuwaalikuwa anachangia mjadala wa wizara kwa kujadili manyanyaso ya
polisi dhidi ya wafuasi wake.
Akichangia mjadala wa kupitisha Bajeti ya Wizara
ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2013/14, Abwao ndiye
alianza kumshambulia Lukuvi baada ya kumtuhumu kuwa alikuwa anatumia
vibaya Jeshi la Polisi kwa kubambikia watu kesi.
Abwao ambaye alitumia nafasi hiyo kuwa atawania
ubunge katika jimbo hilo ili kumng’oa Lukuvi, alisema kuwa wale
wanaomuunga mkono wamekuwa katika kipindi kigumu jimboni humo kutokana
na kunyanyaswa na polisi.
“Lukuvi amezoea kunipachika sifa kuwa mimi ni
mzoefu wa kufungua baa tu, lakini ameshindwa kuzitaja sifa zangu
nyingine kuwa mimi ni mwanamke wa shoka na ni tishio kwenye nafasi yake
ya ubunge.
Pia alimtuhumu Lukuvi kwa kushindwa kupeleka maendeleo katika kipindi cha miaka 10 akiwa Mbunge wa Isimani.
“Jamani watu wa Isimani mnajua wenyewe mmekuwa na
wabunge mawaziri kwa miaka 20, lakini maendeleo hakuna. Umeme unatoka
Kidatu unapita juu ya Isimani na pia barabara ni mbovu,” aliongeza
Abwao.
Naye Lukuvi hakubaki nyuma kwani aliibuka na
kumjibu Abwao kuwa maneno yake ni sawa na ya `mganga njaa’ na aliwataka
polisi wasishtushwe na maneno ya mbunge huyo.
“Kizuri chajiuza, kibaya chajitembeza, inakuwaje
mbunge azungumzie mambo ya Isimani katika mjadala huu wakati watu
wanazungumzia masuala ya muhimu ya Arusha,” alisema Lukuvi akimaanisha
suala la kulipuliwa kwa Kanisa Katoliki huko Arusha.
“Ukiona vyaelea ujue vimeundwa, Isimani umeikuta
na utaiacha, wananchi mjionee wabunge wa Iringa tupo wengi na kila mmoja
anafahamu uwezo wake,” alisema Lukuvi, ambaye pia alisifia polisi na
kusema wale wanaowashutumu basi wana kasoro.
Comments