BAYERN
Munich usiku huu waiadhibu Barca nyumbani na kutinga fainali ya kwanza
ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya ambapo sasa watakutana na Wajerumani
wenzao baada ya kuichapa Barcelona 3-0 kwenye Uwanja wa Nou Camp na
hivyo kusonga mbele kwa jumla ya mabao 7-0.
Mabingwa hao wapya wa Ligi Kuu
ya Ujerumani waliimaliza mechi mapema wiki iliyopita kwa ushindi wa 4-0
nchini Ujerumani na hapakuwa na namna ya kufufuka kwa Wahispania hao
wakati Arjen Robben alipofunga goli la kuongoza dhidi ya kipa Victor
Valdes katika dakika ya 49.
Kudhalilika kwa Barca
kulikamilishwa mwishoni mwa mechi wakati Gerard Pique alipojifunga
mwenyewe na Thomas Mueller, ambaye alifunga magoli mawili katika mechi
yao ya kwanza, akapachika la tatu kwa kichwa.
Barca, kama Bayern ambao
wanafukuzia taji la tano la Ulaya, wanategemea kipaji cha Lionel Messi,
ambaye anarejea kutoka katika majeraha ya misuli ya nyuma ya paja na
ambaye aliachwa benchi, lakini bila ya Mwanasoka Bora wa Dunia huyo
hawakuwa na makali yoyote.
Bayern watacheza dhidi ya
Borussia Dortmund katika mechi ya fainali kwenye Uwanja wa Wembley mjini
London Mei 25 baada ya Dortmund kuitoa Real Madrid kwa jumla ya mabao
4-3 Jumanne.
Comments