BREAKING NEWS.......KANISA LA KATOLIKI ARUSHA LADAIWA KULIPULIWA LEO


Kiongozi  wa kanisa Katoliki ulimwenguni ,Papa Francis
............................................................................
Leo kulikuwa na uzinduzi wa Parokia mpya ya Olasit mjini Arusha. Mgeni rasmi alikuwa Mwakilishi wa Papa toka Vatican. Kulikuwa na wageni wengi waliambatana na mwakilishi wa papa, wakiwemo maaskofu, mapadre na watawa kutoka mataifa mbalimbali.

Mtoto mmoja ameeleza kuwa aliona watu waliokuwa kwenye mini bus wakirusha kitu kuelekea kwenye mkusanyiko wa wakristo waliokuwepo kwenye ibada.

Taarifa zinaeleza kuwa eneo kubwa limetapakaa damu, watu wengi wamejeruhiwa. Inasadikiwa kuwa wapo waliokufa lakini haijathibitika. Muda huu vyombo vyote vya usalama vipo eneo la tukio.

Kwa update zaidi sikiliza Radio Maria http://streema.com/radios/play/6848.

Hivi sasa kuna taharuki kubwa, na kuna taarifa ya milipuko mingine, haijulikani kama ni ya washambuliaji au ya polisi, mbali na eneo la ibada.

Nawapeni pole nyingi waliokumbwa na mkasa huu, wakatoliki, wakristo wote na wanaolitakia amani Taifa letu.


Taarifa  kutoka mkoani Arusha  ambazo  mtandao  huu  wa  www.matukiodaima.com umezipata  zinaeleza  kuwa  kuna mlipuko  mkubwa mfano  wa  bomu umejitokeza katika kanisa la RC Arusha na kujeruhi  baadhi ya waumini.

Mlipuko huo  unadaiwa  kusababisha taharuki  kubwa katika mji  wa Arusha na kuendelea  kuiweka nchi katika hali tete  zaidi .

mwandishi maalum  wa mtandao  huu  kutoka Arusha anasema  kuwa tukio hilo  limetokea katika parokia ya  Olasit  mjini Arusha na bado jitihada za uokoaji zinaendelea  kufanyika.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA