Mtanzania
Hasheem Thabeet(pichani katikati) hivi sasa anazidi kutamba na
kujiimarisha katika kuwa mmojawapo kati ya wanamichezo wazaliwa wa
Afrika waliopo nchini Marekani ambao wanafanya vizuri katika anga za
michezo nchini humo.Hasheem anasoma katika Chuo Kikuu Cha Connecticut akichezea timu yao maarufu ya mpira wa kikapu(basketball) ijulikanayo kama Connecticut Huskies.
Hata
hivyo Hasheem ametoka mbali kama ambavyo unaweza kuona katika picha
hiyo hapo juu.Hapo bado alikuwa jijini Dar akiwa na wasanii wa muziki wa
kizazi kipya,Mandojo na Domokaya.BC inamtakia Hasheem kila la kheri
katika jitihada zake..
Comments