KAMPUNI YA PUMA YAINGIA MKATABA KUIVALISHA ARSENAL
Juu: Logo
ya 'Washika Bunduki' Arsenal FC. Chini: Mashabiki wa soka nje ya Uwanja wa
Emirates jijini London, unaomilikiwa na Arsenal
LONDON,
England
Mkataba wa
sasa wa Arsenal na Kampuni ya Nike, wenye thamani ya pauni milioni 55 kwa miaka
saba – unafikia tamati mwishoni mwa msimu ujao
KLABU ya
Arsenal, imeingia mkataba wa jezi na vifaa vya michezo na Kampuni ya Puma wenye
thamani ya pauni milioni 170, unaohitimisha miaka 20 ya Washika Bunduki hao
kuvalishwa na Kampuni ya Nike.
Mtendaji
Mkuu wa Gunners, Ivan Gazidis ametiliana saini na Puma ya kuivalisha Arsenal kwa
miaka mitano, mkataba unaomaanisha kuwa klabu itapokea vifaa vyenye zaidi ya
pauni milioni 30 kwa mwaka.
Mkataba wa
sasa wa Arsenal na Kampuni ya Nike, wenye thamani ya pauni milioni 55 kwa miaka
saba – unafikia tamati mwishoni mwa msimu ujao.
Arsenal
imekuwa ikikataa mikataba ya muda mrefu tangu ilipohamia kwenye dimba la
Emirates kutoka lile la zamani la Highbury mwaka 2006.
Lakini sasa
imeanga mbele na kujaribu kutanua wigo wa miakataba mipya na yenye
tija.
Nike
ilikuwa ya kwanza kukataa makubaliano ya mkataba mpya Gunners, na kuamua
kutofanya maboresho na nyongeza ya mkataba wa sasa.
Gunners
inayonolewa na Arsene Wenger, ilitangaza na kufuata sera za kubana matumizi yake
kwa kila msimu, tangu ilipohama Highbury, miaka saba
iliyopita.
Sera hiyo
inapingwa na mashabiki wa timu hiyo, wanaoumizwa na ukame wa mataji wa miaka
minane sasa, na wanaona timu yao inaweza kushindana na klabu zinazotumia pesa
kubwa England za Man United, Man City na Chelsea kupitia pesa za
udhamini.
The
Sun
Comments