KUFUATIA MGOMO WA DALADALA IRINGA , SUMATRA YAKUNJUA MAKUCHA SASA YATISHIA KUWATIMUA KAZI MAOFISA WAKE .......

 Mmiliki  wa daladala akiwasilisha kero  yake kwa uongozi wa Sumatra
 Mmoja kati ya madereva hao na mmiliki wa daladala Bw Peter akitoa maoni yake kwa Sumatra.
 Baadhi ya madereva wakitoa maoni yao juu ya kero  wanazozipata
SAKATA  la  mgomo  wa  daladala katika Manispaa ya  Iringa limeanza  kushughulikiwa kwa kasi kubwa na mamlaka ya uthibiti ,usafiri  wa majini na nchi kavu (SUMATRA) makao makuu  baada ya  kutuma maofisa  wake  kutoa elimu kwa wamiliki  huku mamlaka  hiyo ikiapa kuendelea  kupambana madereva wanaonyanyasa abiria kwa kuvunja  wa  sharia.
Pia  imeapa  kuwachukulia hatua kali  ikiwa ni pamoja na kuwafukuza kazi maofisa  wake ambao  watabainika kupokea faini ndogo kinyume na faini  inayopaswa  kulipwa kisheria.
Akizungumza na  wamiliki  wa daladala na madereva leo  katika  ukumbi wa shule ya  Sekondari Lugalo ,  kaimu mkurugenzi wa idara ya usafiri  wa barabarani Bw Leo Ngowi alisema  kuwa ni  vema wamiliki  wa daladala na  madereva kuheshimu  sharia za usafirishaji ikiwa ni pamoja na  kuzitambua sharia  hizo pia  wasiwe nyume  kuwafichua maofisa wanaukula  rushwa .
Ngowi  alisema  kimsingi katika  sharia  za Sumatra  kuna faini  za aina mbili  ikiwemo ya Tsh 500,000 ambapo nusu yake Tsh 250,000 na  faini  nyingine ni Tsh 100,000 na nusu yake ni Tsh 50,000 na  kuwa hakuna faini ya chini ya hapo na iwapo kuna mtendaji anapokea  chini ya viwango  hivyo atafukuzwa kazi mara  moja. 
Pia Alisema kuwa  mamlaka  inapiga   marufuku kwa madereva wa  vyombo  vya usafiri  kupakia wanyama kama mbuzi ,ama mkaa pamoja  na  vitu  vingine  vya  hatari  kwa abiria .
Pamoja na kuapa kuendelea  kusimamia sharia  bado SUMATRA  afisa  huyo alisema   kuwa  utendaji kazi  wake ni masaa 24 hivyo  madereva  wasifikiri kuwa mamlaka  hiyo ina muda  wa  maalum wa kufanya kazi .
 Alisema  kuwa  sheria  hizo  zimewekwa  ili  kuhakikisha kuwa  sekta  hiyo ya usafiri inaboreshwa na  kusiwepo  kwa malalamiko  kutoka pande mbili ya mtoa huduma na mpokeaji wa  huduma  husika.
" Sheria  zinzohusu sekta  ya  usafirishaji ni pamoja na  sharia  ya  viwango ya  mwaka 1975,sheria namba 30 ya  mwaka 1973 ya  usalama barabarani  sharia  namba  1 ya 1973 ya leseni za usafirishaji  na  sharia nyingine nyigi ambazo wanapaswa  kuzitambua"
Hata  hivyo  alisema  kuwa  kwa mujibu  wa sharia  za Sumatra  haziruhusu  kwa daladala  moja ama chombo kimoja cha usafiri  kumiliki  leseni mbili  za njia na kuwa iwapo wapo  wanaofanya hivyo ni kinyume.
Ngowi alisema  kuwa  kitendo  cha daladala  kushusha abiria  njiani hata kama ni abiria mmoja ni kosa na kuwa lengo la usafiri  wa daladala ni kushusha na kupakia na  kuwa kwa kawaida  usafiri  wa mijini huwa haukai sehemu  moja kama ilivyo mabasi ya vijijini ambayo yamekuwa yakiegesha sehemu moja kugonja abiria.
"Hakuna  sharia  inayoruhusu usafiri  wa mjini kukaa sehemu  moja kwa  zaidi ya dakika  20 na  kuwa kwa kawaida  usafiri  wa mjini ni kushusha na kupakia na kuendelea na safari ...,kama  kituo kimoja hakina abiria  basi kituo kinachofuata  kitakuwa na abiria na hata kama kuna abiria wawili ama mmoja haki yake ya msingi kufikishwa hadi mwisho wa safari kwa mujibu wa leseni ya  njia"
Aidha  alisema  kuwa Sumatra imesitisha  utoaji  wa leseni kwa magari  yenye  uwezo  wa  kubeba abiria  kuanzia  7 hadi 12 iwapo yatatumika kwa matumizi binafsi na namba  za usajili ni zile za njano si  vinginevyo .
Ngowi  alisema  kuwa upande wa madereva ni lazima  kabla ya kuanza kazi kumfahamu vema mmiliki wa gari analoliendesha ikiwa ni pamoja na anuani na namba  za simu .
Pia  aliwataka madereva  kukataa kuendesha gari iwapo litabainika  kuwa ni linaloweza kuhatarisha usalama  wake na abiria  wake .
Hata  hivyo alisema  kuwa ni  wajibu kwa mmiliki wa gari  kumtafutia abiria wake chakula  iwapo gari  hilo  litaharibika kwa zaidi ya masaa mawili na kuendelea  ama sehemu ya kulala  iwapo gari  hilo halitaendelea na  safari na sharia  hiyo kwa magari yanayofanya  safari ndefu  kwa  maana ya mikoa.
Wakati  kwa  upande  wa  daladala  ni marufuku  kusimama kituoni kwa zaidi ya dakika 5 katika  kituo  kimoja na kufanya  hivyo ni kosa  kisheria.
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji  wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Terresia Mahongo alisema  kuwa  lazima  Sumatra  kuweka mkakati  wa kuwasaidia wananchi ambao  wameendelea  kupata kero  kubwa ya  usafiri kwa madereva  wa daladala kuwakalisha  abiria kwa muda mwingi eneo la posta .
Kuhusu suala la kukosekana kwa choo katika eneo la Isakalilo alisema  kuwa anawahakikishia madereva hao kuwa lazima kero  hiyo ataifanyia kazi ikiwa ni pamoja na kujenga  choo mapema  zaidi  eneo hilo . 
Wakati madereva  hao  walilalamikia  suala la ubovu  wa barabara  kuwa  baadhi ya njia kama ya Mikimbizi  daladala  zimekuwa  zikikwepa  kwenda huko kutokana na njia  hiyo kuwa na mawe mengi na njia kuwa mbovu kupita kiasi hivyo wanataka suala la njia  kurekebishwa  zaidi.
Huku mkurugenzi  wa Manispaa ya  Iringa akiahidi kutengeneza barabara  hizo ndani ya wiki mbili zijazo ili kuwa na barabara  nzuri  zaidi.
Wakati  huo  huo mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa Bi.Mahongo amekataa ombi la madereva na  wamiliki wa daladala mjini Iringa la kutaka kikao kijacho  kati ya wadau wa usafiri na madereva na Manispaa kukutana majira ya saa 2 usiku na kuwa kwa muda  huo hawapo tayari kufanya  hivyo.
" Mnataka  tukutane usiku  ili iweje pia na mimi ni kiongozi wa umma ninalindwa na sharia  za utumishi  wa umma sasa mkisema tukutane usiku sitakuwa tayari labdala iwe saa 10 jioni kama ambavyo baadhi yenu mmependekeza iwe saa 10 jioni siku ya jumapili nipo tayari "
Hivyo alisema kikao hicho kitakuwa cha wamiliki pekee wa daladala na si vinginevyo huku akidai kuwa lazima  chama cha madereva wa daladala mjini Iringa kuchunguzwa upya kwani ndicho chanzo cha yote haya.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI