RAIS KIKWETE AKATIZA ZIARA NCHINI KUWAIT KUTOKANA NA SHAMBULIO LA KIGAIDI LA MLIPUKO WA BOMU KATIKA KANISA LA KATOLIKI ARUSHA
THE UNITED REPUBLIC
OF TANZANIA
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512,
2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
Fax: 255-22-2113425 |
|
PRESIDENT’S OFFICE,
THE
STATE HOUSE,
P.O. BOX
9120,
DAR
ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo,
Jumatatu, Mei 6, 2013, ameamua kukatiza ziara yake ya Kiserikali nchini Kuwait ili
kurejea nyumbani kutokana na tukio la shambulio la kigaidi la mlipuko mjini
Arusha ambako watu wawili wamefariki na 60 wamejeruhiwa.
Rais Kikwete aliyekuwa aondoke kesho kurejea
nyumbani, amelazimika kukatiza ziara hiyo na anaondoka Kuwait
City kurejea nyumbani mara moja ili
kuwa karibu na wafiwa pamoja na wale waliojeruhiwa katika shambulio hilo la kigaidi.
Miongoni mwa shughuli ambazo hazitafanyika
sasa kutokana na uamuzi huo wa Rais ni ziara ya kutembelea Kampuni ya Mafuta ya
Kuwait katika eneo la Ahmadi mjini Kuwait. Aidha,
Rais hatahudhuria dhifa ya chakula cha jioni ambacho alikuwa anaandaliwa na
Waziri Mkuu wa Kuwait,
Mheshimiwa Sheikh Jaber Al Mubarak Al Hamad Al Sabah.
Imetolewa na:
Kurugenzi
ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
6 Mei, 2013
Comments