Rais Jakaya Kikwete akipita katikati ya wachezaji wa Taifa Stars tayari kwa tukio la kupiga picha nao, Ikulu, Dar es Salaam.PICHA ZOTE NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA)
Rais Jakaya Kikwete (mstari wa mbele katikati) akiwa na wachezaji wa timu ya soka ya Taifa (Taifa Stars), pamoja na wajumbe wa Kamati ya Ushindi ya Taifa Stars Ikulu, Dar es Salaam leo, ambapo aliwaita kula nao chakula cha mchana na kuwapa hamasa ya ushindi dhidi ya Morocco na mechi zingine watakazokabiliana nazo katika michuano ya kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia 2014
Wachezaji wakipata chakula cha mchana walichoandaliwa na Rais Kikwete, Ikulu, Dar es Salaam
Rais Jakaya Kikwete akizungumza na wanakamati ya ushindi wa Taifa Stars, Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Dk. Fnella Mkangara pamoja na Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen.
Wachezaji wa Taifa Stars wakimsikiliza Rais Kikwete alipokuwa anazungumza nao baada ya chakula
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo akizungumza kabla ya kumkaribisha Rais
Rais Jakaya Kikwete akiwapa hamasa wachezaji wa timu hiyo
Nahodha wa Taifa Stars, Juma Kaseja akiahidi mbele ya Rais Jakaya Kikwete kwamba watafanya juu chini kupata ushindi katika mechi zote zilizobakia.
Rais Jakaya Kikwete (katikati) na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodger Tenga (kulia) pamoja na Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Ushindi ya Taifa Stars, Dk. Ramadhan Dau wakifurahi baada ya Nahodha wa Taifa Stars, Juma Kaseja kuahidi ushindi dhidi ya Morocco.
Kocha Mkuu wa Tgaifa Stars, Kim Pousen akiahidi ushindi mbele ya Rais
JK akiagana na Rais wa Shurikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodger Tenga
JK akiagana na mjumbe wa Kamati ya Ushindi ya Taifa Stars, Teddy Mapunda
JK akiagana na Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania, Dioniz Malinzi
JK akiagana na George Kavishe mjumbe wa Kamati ya Ushindi ya Taifa Stars na Meneja wa bia aina ya Kilimanjaro wadhamini wakuu wa Taifa Stars.
Rais akiagana na wachezaji wa Taifa Stars
Rais Jakaya Kikwete (mstari wa mbele katikati) akiwa na wachezaji wa timu ya soka ya Taifa (Taifa Stars), pamoja na wajumbe wa Kamati ya Ushindi ya Taifa Stars Ikulu, Dar es Salaam leo, ambapo aliwaita kula nao chakula cha mchana na kuwapa hamasa ya ushindi dhidi ya Morocco na mechi zingine watakazokabiliana nazo katika michuano ya kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia 2014
Wachezaji wakipata chakula cha mchana walichoandaliwa na Rais Kikwete, Ikulu, Dar es Salaam
Rais Jakaya Kikwete akizungumza na wanakamati ya ushindi wa Taifa Stars, Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Dk. Fnella Mkangara pamoja na Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen.
Wachezaji wa Taifa Stars wakimsikiliza Rais Kikwete alipokuwa anazungumza nao baada ya chakula
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo akizungumza kabla ya kumkaribisha Rais
Rais Jakaya Kikwete akiwapa hamasa wachezaji wa timu hiyo
Nahodha wa Taifa Stars, Juma Kaseja akiahidi mbele ya Rais Jakaya Kikwete kwamba watafanya juu chini kupata ushindi katika mechi zote zilizobakia.
Rais Jakaya Kikwete (katikati) na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodger Tenga (kulia) pamoja na Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Ushindi ya Taifa Stars, Dk. Ramadhan Dau wakifurahi baada ya Nahodha wa Taifa Stars, Juma Kaseja kuahidi ushindi dhidi ya Morocco.
Kocha Mkuu wa Tgaifa Stars, Kim Pousen akiahidi ushindi mbele ya Rais
JK akiagana na Rais wa Shurikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodger Tenga
JK akiagana na mjumbe wa Kamati ya Ushindi ya Taifa Stars, Teddy Mapunda
JK akiagana na Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania, Dioniz Malinzi
JK akiagana na George Kavishe mjumbe wa Kamati ya Ushindi ya Taifa Stars na Meneja wa bia aina ya Kilimanjaro wadhamini wakuu wa Taifa Stars.
Rais akiagana na wachezaji wa Taifa Stars
Na Veronica Kazimoto –MAELEZO
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo
amekutana na timu ya Taifa (Taifa stars) kwa lengo la kuitia moyo katika
mechi ijayo kati yake na timu ya Moroco ikiwa ni harakati za Tanzania
kutafuta tiketi ya kucheza fainali za kombe la Dunia kwa mara ya kwanza
mwaka 2014.
Rais
Kikwete ameiambia timu hiyo kuwa ina uwezo mkubwa wa kusonga mbele
kutokana na uwezo mkubwa waliouonesha katika mchezo wao dhidi ya Gambia
ambapo walifanikiwa kupata ushindi wa bao 2-0.
“Maadamu
mara ya kwanza mliwashinda Gambia, hakikisheni pia mnapata ushindi
dhidi ya Moroco, mkishinda tunafurahi sana na mkishindwa tunanyong’onyea
sana,” amesema Rais Kikwete.
Aidha
amempongeza kocha wa timu hiyo Kim Poulsen pamoja na Kamati ya Taifa
ya ushindi ya Taifa stars kwa kuisaidia timu hiyo kiasi cha shilingi
milioni 30 ikiwa ni mkakati wa kuiongezea nguvu kwa hatua iliyofikia na
kuwataka wachezaji kujituma ili kuwafurahisha watanzania ambao hivi
sasa wanaipenda timu yao ya Taifa.
Nae
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Fenera Mukangara amesema
Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa michezo nchini
ili kuondoa changamoto zinazoikabili timu hiyo.
Kwa
upande wake Kocha Poulsen, amemshukuru Rais Kikwete kwa kuwakaribisha na
kuwatia moyo ambapo ameahidi kuifundisha vizuri timu hiyo ili
kuhakikisha kuwa wanapata ushindi.
Akizungumza
kwa niaba ya wachezaji wenzake nahoidha wa timu hiyo Juma Kaseja
amemshukuru Rais Kikwete na kuahidi kujituma kwenye mazoezi na hatimaye
kuibuka washindi kwenye mechi zijazo.
Taifa stars ambayo inakamata nafasi ya pili katika kundi C inatarajia kucheza ugenini na Morocco mnamo Juni 7 mwaka huu.
Comments