TUDUMISHE UAFRIKA WETU

Pichani ni viongozi wa taifa letu mwanzoni kabisa mara tu baada ya kupata uhuru mwaka 1961.Jambo moja ambalo limetuvutia mpaka kuamua kuweka kumbukumbu hii ni mavazi ya “waheshimiwa”.Ukitizama utaona kwamba kumbe wakati tunapata uhuru,wengi miongoni mwa viongozi wetu,walikuwa wanathamini mavazi ambayo hata kwa kuyatizama tu unaweza kutambua kwamba ni mavazi ya “kiafrika”.
Sasa nini kilitokea baada ya hapo?Mbona leo hii ni nadra sana(kama huwa inatokea) kuwaona viongozi wetu wakitukuza mila,tamaduni na desturi zetu japo kuanzia kwenye mavazi tu?Mbona wenzetu wa sehemu zingine za Afrika kama vile Afrika Magharibi wao wanaendelea kujinadi na mavazi yao ya asili?Ni kweli kwamba sisi hatuna vazi la taifa au tumezembea tu kuwa nalo?
Je unawatambua viongozi unaowaona pichani?Kama jibu ni ndio basi tusaidiane katika kuweka kumbukumbu sawa.Shukrani za pekee kwa Michuzi kwa kuhifadhi picha za kumbukumbu kama hizi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.