UMISSETA MBEYA YAFUNGULIWA KWA MAJONZI MAKUBWA

Afisa elimu mkoa wa Mbeya Juma Kaponda amemtaja marehemu kuwa mtu aliyekuwa na mchango mkubwa katika ufundishaji wa somo la hisabati shuleni hapo na pia usimamizi wa shughuli za michezo.
Afisa michezo mkoani hapa George Mbijima amesema wamepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha mwalimu Chalo kwakuwa kilitokea ikiwa ni muda mfupi umepita tangu walipokuwa katika kikao cha pamoja kabla hajawaacha na kwenda kushughulikia shughuli ya ugawaji chakula kwa washiriki wa mashindano na kisha kuanza safari kurudi nyumbani kwake.
Baadhi ya wanafunzi washiriki wa mashindano ya wanafunzi wa shule za sekondari(UMISETA) mkoani Mbeya yanayoendelea katika viwanja vya Sekondari ya Iyunga pamoja na Viongozi wakifuatilia hotuba ya afisa elimu mkoani hapo Mwalimu Juma Kaponda kabla ya kufungua mashindano hayo leo.



MASHINDANO ya wanafunzi wa shule za sekondari(UMISETA) mkoani Mbeya yamefunguliwa kwa simanzi kubwa baada ya mmoja wa waratibu wa mashindano hayo kupoteza maisha katika ajali. Aliyepoteza maisha usiku wa kuamkia leo ikiwa ni siku moja baada ya kuanza kwa mashindano hayo ni mwalimu Abdalah Chalo(41) wa shule ya sekondari Iyunga ya jijini hapa aliyegongwa na lori wakati akiendesha pikipiki alipokuwa akirudi nyumbani kwake muda mfupi baada ya kukamilisha zoezi la kugawa chakula kwa washiriki wa michezo. 

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoani Mbeya Diwani Athuman mwalimu Chalo aliyekuwa akiendesha pikipiki yenye namba T 815 BKQ aina ya King Fan alikutwa na mauti baada ya kugongwa na lori lenye namba T 441 BYW aina ya Scania likiwa na tela lenye namba T 496 BWD. Kamanda Athuman amesema tukio hilo lilitokea Mei 22 majira ya saa 3:00 ya usiku katika eneo la Iyunga darajani jirani na nyumbani kwa marehemu na kumtaja dereva wa lori kuwa ni Heri Faustin(35) mkazi wa eneo la Mama John jijini Mbeya.

 Akifungua mashindano ya Umiseta alhamisi hii katika viwanja vya shule ya sekondari Iyunga,afisa elimu mkoa wa Mbeya Juma Kaponda amemtaja marehemu kuwa mtu aliyekuwa na mchango mkubwa katika ufundishaji wa somo la hisabati shuleni hapo na pia usimamizi wa shughuli za michezo.

 Naye afisa michezo mkoani hapa George Mbijima amesema wamepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha mwalimu Chalo kwakuwa kilitokea ikiwa ni muda mfupi umepita tangu walipokuwa katika kikao cha pamoja kabla hajawaacha na kwenda kushughulikia shughuli ya ugawaji chakula kwa washiriki wa mashindano na kisha kuanza safari kurudi nyumbani kwake.

 Mashindano ya Umiseta kwa mkoa wa Mbeya mwaka huu yanashirikisha jumla ya wanafunzi 1 kutoka halmashauri 1066 za mkoani hapa lengo likiwa ni kupata wanafunzi 125 watakaounda timu ya mkoa kwaajili ya kushiriki mashindano hayo katika ngazi ya kanda.

Picha na Mbeya yetu

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI