WANANCHI KUSAFIRI TOKA MTWARA HADI BUKOBA KWA LAMI


1
DR. JOHN MAGUFULI

Na Immaculate Makilika- Dodoma
WANANCHI wataweza kusafiri kutoka Mtwara  hadi Bukoba  kwenye  barabara  ya lami,hayo yamesemwa  mapema leo  hapa Bungeni Mjini Dodoma  wakati  Waziri wa Ujenzi  John Magufuli alipokua akijibu  swali la Martha Mlata(Viti Maalum-CCM), swali lililohoji  juu ya ahadi ya Serikali katika kipindi cha awamu ya nne na ahadi hiyo iliyosema  wananchi wataweza kusafiri  kwa taxi  toka Mtwara  hadi Bukoba,Je utekelezaji   wa ahadi hiyo umefikia wapi.Aidha Waziri Magufuli  alisema kuwa nia ya msemo huo ni kuonesha kwamba wananchi  wataweza kusafiri  toka  Mtwara hadi Bukoba  kwa lami na kuongeza kuwa lengo hilo limetekelezwa  kwa mafaniko makubwa hadi kufikia asilimia 99  ya barabara  yote kutokea Mtwara hadi Bukoba.
Hata hivyo Magufuli aliendelea kwa kwa kusema kwamba barabara  yote kuanzia  Mtwara  – Dar es Salaam- Dodoma-Singida- Nzega-Tinde-Usagara pamoja na Geita-Bwanga-Kyamyorwa hadi Bukoba yenye urefu  wa kilometa zipatazo 1,989 imejengwa kwa kiwango cha lami.
Isipokua sehemu fupi  yenye urefu wa takribani  kilometa  26 katika barabara ya Ndundu-Somanja ambayo itakamilika kujengwa kwa kiwang o cha lami kabla ya Desemba,2013
Serikali ya awamu ya nne itahakikisha  ahadi ya wananchi kusafiri kwenye barabara ya lami toka Mtwara hadi Bukoba inatekelezwa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA