Airtel yaongeza muda vifurushi vya Airtel Yatosha, sasa huduma masaa 25 kwa siku
Airtel
Tanzania imeendelea kutimiza dhamira yao ya kuwapatia wateja wake
unafuu zaidi kupitia huduma yake ya AIRTEL YATOSHA nchini ambapo sasa
wateja watafurahia Vifurushi vya Airtel Yatosha kwa masaa 25 kwa
siku, hii itawawezesha watanzania kufurahia kupiga simu mtandao wowote
kwa gharama nafuu kwa muda mrefu zaidi.
Akiongea
wakati wa uzinduzi wa Airtel yatosha masaa 25 Meneja Uhusiano wa Airtel
Jackson Mmbando alisema” kuanzia sasa, huduma ya Airtel yatosha kwa
siku itakua kwa masaaa 25 kuanzia pale mteja anapojiunga na huduma,
yaani masaa 24 ya kuongea na kama vile haitoshi Airtel yatosha
inakuongezea saa jingine moja la ziada. Sasa wateja wa Airtel watafurahi
kupiga simu kwa gharama nafuu na kwa muda zaidi kuliko ilivyokuwa
awali”.
“Hii
ni ya kwanza na pekee kutoka Airtel, Airtel yatosha itaendelea kuwa
suluhisho la mawasiliano ya huduma za simu kwa watuamiaji na wateja wa
Airtel nchi nzima ”. aliongeza Mmbando
Airtel
yatosha ni huduma iliyoanzishwa ili kuleta kuvunja mipaka kwa
watanzania na kuwawezesha kuwasiliana ndani na nje ya mtandaa kwa
gharama nafuu. Kujiunga na huduma hii piga *149*99# na atapata majibu papo hapo achague unataka Yatosha WIKI au Yatosha SIKU au Tosha ya Mwenzi.
Comments