AMA KWELI HIZI NI DALILI ZA MWISHO ,KIJANA AKAMATWA MSIKITINI AKITAKA KUMTAPELI IMAMU NA WAUMINI IRINGA

 Kijana Wiliam Daud a.k.a  Hassan Idd Lumbanga (jina la  kutapeli) mkazi  wa Majengo mkoani Katavi akiwa chini ya ulinzi ndani ya msikiti wa Ijumaa -Miyomboni mjini Iringa baada ya  kushitukiwa kuwa ni tapeli aliyetaka kumtapeli Imamu  wa msikiti  huo wa waumini  wake  leo 
 Waumini  hao wakifanya mawasiliano na polisi baada  huku tapeli huyo  kulia akiwa katika hofu kubwa 
 Naibu imamu wa masikiti wa Ijumaa - Miyomboni Issa Boki ( kushoto) akiongozana na  baadhi ya  waumini wa msikiti  huo kumweka  chini ya ulinzi tapeli  huyo (katikati mwenye shati la kijani ambae alitaka  kutapeli kiasi cha  Tsh 55,200 zilizochangwa na  waumini kwa ajili ya kijana  huyo kabla ya  kubaini kuwa ni tapeli  hapa  wakimpeleka  polisi 
 Huyu  ndie  Kijana Wiliam Daud a.k.a  Hassan Idd Lumbanga (jina la  kutapeli) mkazi  wa Majengo mkoani Katavi  aliyeingia msikitini  kufanya utapeli leo 
  Kijana Wiliam Daud a.k.a  Hassan Idd Lumbanga (jina la  kutapeli) mkazi  wa Majengo mkoani Katavi  akiwa  chini ya ulinzi ,kulia ni katibu wa msikiti huo Juma Kibasila aliyeshika  kichwa 

 Kijana  huyo tapeli  akipelekwa  polisi  na  waumini wa msikiti wa Ijumaa -Miyomboni leo  kushoto ni katibu wa msikiti  huo Juma Kibasila 
Waumini  wa  dini ya kiislamu katika msikiti  wa Ijumaa - Miyomboni mjini Iringa  wakimfikisha  polisi  kijana aliyevaa shati la kijani baada ya  kuingia ndani ya msikiti kwa  lengo la kufanya utapeli 

....................................................................................................................................................

IKIWA ni siku chache zimepita  toka  kuumbuliwa kwa tapeli mzee aliyekuwa akijifanya hana mikono katika  eneo ya Mikyomboni mjini Iringa ,wimbi la utapeli  laendelea  kutikisha  mkoa  wa Iringa baada ya  matapeli hao  kuja na mbinu mpya  ya  kuingia katika nyumba za ibada na kuwatapeli  waumini .

Mbinu  hiyo  imebainika  leo katika msikiti  wa Ijumaa - Miyombini baada ya  waumini  wa msikiti  huo  kumnasa  kijana Wiliam Daud mkazi  wa Majengo mkoani Katavi ambae amekuwa akifanya kazi ya  utapeli katika misikiti mbali mbali hapa nchini kwa  kutumia jina la    Hassan Idd Lumbanga (jina la  kutapeli) ambalo amekuwa akilitumia misikitini pekee.

Kama  ilivyo ada  siku  zote za mwizi ni arobaini basi  hivi ndivyo ilivyokuwa  kwa kijana  huyo baada ya jana  kufika katika msikiti  huo na  kuungana na  waumini  wake katika swala na  wakati  shughuli  hizo za swala  zikiwa katikati kwa naibu imamu  wa msikiti  huo Issa Boki akiendelea  kuongoza  waumini hao ghafla  kijana  huyo tapeli alijiangusha  chini mfano wa mtu aliyezidiwa na kupoteza fahamu .

Hali  hiyo  iliwalazimu  waumini hao  kusitisha shughuli za ibada na  kutafuta  gari haraka haraka na kumkimbiza  katika Hospitali ya mkoa  kijana  huyo tapeli .

Alisema naibu  imamu  huyo Issa Boki alipozungumza na mtandao  huu  wa www.matukiodaima.com  kuwa baada ya  kufika Hospitali ya  Rufaa ya mkoa  wa Iringa kijana  huyo alitakiwa kulazwa kutokana na  kuonyesha  kuzidiwa  zaidi.

Hata  hivyo  baada ya  wao  kuondoka  Hospitali hapo na kijana  huyo  kupelekwa wodini  kulazwa inadaiwa alionekana ni mtu kama mwenye utindio wa ubongo kutokana na vurugu alivyokuwa akiwafanyia  wagonjwa  wenzake kiasi  cha kuhamishwa na kupelekwa katika wodi  la vichaa ambako pia alifanya vurugu kubwa  na kufanikiwa  kutoroka wodini hapo.

Alisema  kuwa katika hali  ya  kushangaza ni pale tapeli  huyo aliporudi tena msikitini hapo leo na  kuungana na  waumini hao katika swala ya mchana  wa  leo na  kuwaomba  waumini  hao  kumsaidia fedha  ili kurejea kwao Katavi .

Kutokana na maombi hayo  Naibu Imamu  huyo aliwaomba  waumini  wake  kumchangia  fedha  na  kupatikana kiasi cha Tsh 55,200 na  wakati  wakijiandaa kumkabidhi  fedha  hizo mmoja kati ya  waumini aliweza kumtambua  kijana  huyo  kuwa ni tapeli ambae amekuwa akitumia mbinu  hizo na kwa mara ya mwisho  alikuwa jijini Dar es Salaam katika msikiti mmoja na kunusurika  kichapo kwa utapeli  huo wa kujiangusha na baada ya siku moja kurejea  kuomba  fedha ili arejee kwao.

Katibu  wa Msitiki  huo Juma Kibasila alisema  kuwa fedha  hizo hawajaweza kumkabidhi tapeli huyo baada ya kumhoji na  kukiri  kuwa si mgonjwa ila amekuwa akiendesha maisha yake kwa  kutapeli  katika  nyumba  mbali mbali za ibada kwa  kutumia mbinu  hiyo ya kujiangusha kama mgonjwa .

Kibasila alisema  kuwa  kwa ujumla  waumini  wa dini  ya Kiislamu ni  watu  wa  kujitolea kwa watu wenye shida na kuwa iwapo kijana  huyo angefika na kuomba msaada kama msaada  bila  kutumia mbinu ya utapeli kama  hiyo hakukuwa na tatizo ila kutokana na utapeli huo  wamelazimika  kumfikisha  polisi  kutokana na kudai kuwa ana miliki funguo malaya  zinazofungua milango mbali mbali ya nyumba na magari hivyo wanahisi ni mtu hatari zaidi .

Kijana  huyo baada ya  kuhojiwa na mtandao  huu alikiri  kuwa ni tapeli anayetafuta maisha kwa mbinu hiyo na  kuwa amefanya utapeli  huo katika misitiki ,makanisa na maeneo mengine yenye mikusanyiko ya  watu wengi na kusaidia na  kuwa  kila anapofanya utapeli kama  huo huwa hakosi kiasi kati ya Tsh 50,000 hadi 500,000 kwa tukio  moja .

Hata  hivyo  alisema katika Misitiki amekuwa akitumia jina  hilo la Hassan Idd Lumbanga ila anapokwenda makanisani amekuwa akitumia jina la Wiliam Daud .

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA