BENKI YA NMB YAFADHILI MAONYESHO YA UBUNIFU WA WATOTO
Benki
ya NMB imefadhili maonyesho ya ubunifu wa watoto waliokusanywa na
Tanzania Mitindo House. Maonyesho ambayo yatahusisha shughuli mbali
mbali za kazi za mikono ambazo watoto wenye vipaji wamekua wakizifanya.
Maonyesho haya yataanza tarehe 8 Juni hadi tarehe 9 juni 2013 kuanzia
saa 9 hadi saa 2 usiku pale Tanzania Mitindo House. Kwa msaada wa benki
ya NMB, watoto hawa watauza kazi zao na kujipatia fedha ambazo
zitawekwa moja kwa moja kwenye akaunti zao za NMB. Fedha hizi
zitawasaidia watoto hawa katika kuendeleza maisha yao ya kila siku hasa
kielimu.
Tanzania
Mitindo House ni Taasisi isiyo ya kiserikali ambayo imedhamiria
kukusanya na kuendeleza Vipaji vya watoto yatima ambavyo vingedidimia
bila msaada wowote.
Watoto hawa wanawakaribisha watu wote waweze kutembelea maonyesho ya kazi za mikono yao.
Mtoto
Frank kutoka nyumba ya watoto Yatima Tanzania Mitindo House akionyesha
umahiri wa kuchanganya rangi katika michoro tofauti tofauti.Frank
anauwezo wa kuona lakini hana uwezo wa kusikia vizuri ni mtoto mwenye
kipaji ajabu.
Comments