CHAGUZI ZAGEUZWA ULINGO WA DAMU.
Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wilayani Kilolo, Lunyiliko Nyaulingo.
YUMKINI hali si shwari tena nchini, baada ya jana chaguzi mbalimbali za kuziba nafasi za udiwani kutawaliwa na matukio ya vurugu na umwagaji damu.
Katika maeneo mbalimbali zimeripotiwa vurugu hizo ambazo ziliwahusisha mashabiki na makada wa CCM na CHADEMA.
Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (CHADEMA), alishambuliwa na vijana wa CCM na kulazimika kulazwa katika hospitali ya Selian mkoani Arusha.
Nasari alijeruhiwa katika vurugu zilizotokea katika kituo cha kupigia kura cha Zaburi, Kata ya Makuy
Comments