JESHI LA POLISI MBEYA LAMSHIKILIA KIJANA KWA KOSA NA KUUA KWA KISU BAADA YA KUTANIWA KUNUNUA BODA BODA MBOVU


 
IGP Mwema
........................................................................................................
Na Esther Macha, Mbeya
JESHI la polisi Mkoani Mbeya linamshikilia Mkazi wa kijiji cha Saman’ombe wilayani Momba Mkoani hapa livingstone mulyatete (42) kwa kosa la kumuua kwa kumchoma kisu Patrick Yohana (30)baada ya marehemu kumtania mtuhumiwa kuwa amenunua piki piki mbovu.
Akizungumza na waandishi wa habari  Kaimu Kamanda wa polisi Mkoani hapa Bw. Barakael Masaki alisema kuwa tukio hilo limetokea juni 26 mwaka huu majira ya saa 12.30 mchana katika kijiji cha Samang’ombe .
Bw. Barakael alisema kuwa chanzo cha ugomvi huo kati ya marehemu na mtuhumiwa ni ugomvi uliotokea kati yao baada ya marehemu kumtania mtuhumiwa kuwa piki piki yake ni mbovu ndipo alipochukua kisu na kumchoma katika ubavu wa kulia na kusababisha kifo chake papo hapo.
Alisema kuwa taratibu zinafanywa ili mtuhumiwa aweze kufikishwa mahakamani mara moja na kujibu tuhuma hizo dhidi yake.
Aidha Kamanda Masaki ametoa wito kwa jamii kudhibiti hasira zao ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza.
Mwisho.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA