Kila la kheri Taifa Stars: Nape.
Chama
Cha Mapinduzi (CCM) kimeitakia kila la kheri timu ya Taifa Stars ambayo
inacheza kutafuta tiketi ya kucheza kombe la dunia mwaka 2014.
Taifa Stars katika mechi yake ya kesho itavaana na Timu ya taifa ya Morocco.
Akizungumza
kutoka Dar es salaam ,Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndg. Nape Nnauye
alisema CCM inaitakia kila lakheri Taifa Stars na mafanikio katika
mchezo wa kesho na kwamba CCM inatambua umuhimu wa taifa Stars kushinda
mechi hiyo ya kesho.
Alisema
anaamini dua za CCM na Watanzania wote zitaiwezesha Taifa Stars
kushinda mechi yake dhidi ya Morocco. "Watanzania tunaomba muiombee
Taifa Stars, tunaimani nayo, bila shaka itashinda kesho" alisisitiza
Nape
Nape Moses Nnauye
The CCM Secretary for Ideology & Publicity
Comments