MAKAMU WA RAIS DKT. BILLAL AONGOZA KILELE CHA SIKU YA MAZINGIRA KITAIFA NAMANYERE MKOANI RUKWA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Billal akihutubia wananchi katika viwanja vya sabasaba Mji mdogo wa Namanyere Mkoani Rukwa katika kuhitimisha siku ya mazingira duniani ambayo kitaifa imefanyika Mkoani Rukwa jana tarehe 05.06.2013. Katika hotuba yake hiyo alisisitizia juu ya uhifadhi wa mazingira kwa kutunza vyanzo vya maji, milima na misitu ya asili, kuhifadhi ardhi na kupanda miti katika maeneo yaliyoathirika na usafi wa mazingira kwa ujumla.

Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Billal akikagua kitalu cha miche ya miti mbalimbali ya mjasriamali ndugu Kidevu (kushoto) katika maonyesho kwenye kilele cha siku ya mazingira kitaifa Mkoani Rukwa katika Mji mdogo wa Namanyere wilayani Nkasi jana tarehe 05.06.2013, Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Dkt. Terezya Luoga Huvisa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI