MAMA ALIYEKAA JUU YA PAA KUPINGA NYUMBA YAKE KUUZWA NA BANK!!

Huyu mama alikaa juu ya paa kwa siku tatu tangu jumamosi kupinga nyumba yao kuchukuliwa na bank.Anasema mumewe alimdhamini mtu alipochukua mkopo bank miaka mingi iliyopita na kushindwa kulipa mkopo huo.
 Kwa mujibu wa maelezo yake kesi yao bado ipo mahakamani kwani tayari yule mdaiwa kuna mali zake zilizotaifishwa.
Mdaiwa alikopa ml 240 wameuza nyumba zake 2 na mabasi mawili.Wenyewe wanachodai katika hilo deni imebaki tsh ngapi na wao watoe?kama nyumba iuzwe watoe deni la bank na hela inayobaki wabaki nayo wao.
Nyumba ipo mbezi Tangi bovu na inaeneo kubwa sana mama anasema hata akiuza si chini ya ml 500 iweje atolewe kwa ml 240?wakati mdaiwa nyumba zake mbili zimeshachukuliwa na mabasi mawili yale makubwa ya safari za mikoani.Hiyo ml 240 haijatimia tu?na kama bado kiasi gani kimebaki?
Ndani ya nyumba vitu walishachukua hao watu wa auction mart  ndani kweupe.Na wakati haya yakiendelea hakukuwa na amri yoyote iliyotoka mahakamani wala hawakuwa na kibali cha mahakama.
Gea alimfata huko huko juu kumsikiliza na tumemsikia leo kwenye heka heka.Kesho pia itaendelea.
Hapa mabaunsa wakimfukuza
Wamemshika
Wamempa kanga nyingine 2 ajifunge maana hakuwa na nguo zaidi ya hiyo kanga moja.
Eneo la nje kulivyokuwa
 Nje ya geti la hiyo nyumba
Chumba cha habari cha clouds fm kimeenda kufatilia hapo bank ya Tanzania Investment bank(TIB)kujua kulikoni??
Maana wakati haya yakiendelea hiyo jana inasemekana hii nyumba imeshauzwa.Inauzwaje na shauri lipo mahakamani?Na jana mume wa huyu mama alikuwa mahakamani maana ilikuwa siku ya kesi kuendelea kusikilizwa.
Na mumewe alirudi na oda maalum kutoka mahakamani kuwa nyumba hiyo isiguswe na vitu vyao virudishwe. PICHA ZOTE KWA HISANI YA DINA MARIOS BLOG

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*