MAVETERANI WAONESHANA UBABE UKONGA!
Mbunge wa jimbo la Ukonga Eugene Mwaiposa akimkabidhi jezi kapteni wa timu ya vijana wa CCM wa jimbo hilo Abubakari (fulana ya bluu) wakati walipoalikwa kwenye bonanza la maveterani wa jimbo hilo. |
Wazee
wa jimbo la Ukonga wakipambana kumkamata kuku
wakati wa bonanza la jimbo hilo mwishoni mwa wiki.
|
Wazee
wa jimbo la Ukonga wakipambana kumkamata kuku
wakati wa bonanza la jimbo hilo mwishoni mwa wiki.
|
Tulia hapa! |
BONANZA la Maveterani jimbo la Ukonga
limefanyika mwishoni mwa wiki na kushuhudia maveterani waalikwa kutoka
Sinza timu yenye Star wengi wa zamani ya Golden Bush wakiibuka mabingwa
wa mchezo wa Soka.
Bonanza hilo lililoandaliwa na
Mbunge wa Jimbo hilo Eugene Mwaiposa lilizikutanisha timu zipatazo kumi
za jimbo hilo na timu mbili zilialikwa kwenye Bonanza hilo.
Ushindani kwenye michuano hiyo ulikuwa mkali ambapo wenyeji wa mashindano hayo timu ya Pugu ilitinga fainali na kupambana na timu ya Golden Bush ya Sinza iliyojaza nyota kama Salum Sued Kusi, Abuu Mtiro na Amani Simba.
Hata hivyo haikuwa kazi rahisi kwa mastaa
hao kupata ubingwa huo kwa vijana wa pugu hadi pale ilipofikia
changamoto ya mikwaju ya Penalt 5, ambapo Golden Bush walipata Penalt
saba kwa 6,
kutokana na kumaliza muda wote wa mchezo bila kufungana.
Kivutio kikubwa kwenye bonanza hilo
kulikuwa kwa mwanamuziki wa kizazi kipya KR Mulla, alipoingia kwa upande
wa timu ya Golden Bush na kufanikiwa kuunganisha kross kali na kupiga
bao ambapo alishangalia kwa Staili ya mapanga Shaa! na kurusha miguu
juu.
Comments