MCHEZAJI WA KIMATAIFA WA CROATIA AFIA UWANJANI

 Alen Pamic aliyelala, akipatiwa huduma ya kwanza na wachezaji wenzake katika moja ya mechi alizowahi kuzimia uwanjani hivi karibuni kutokana na matatizo ya moyo.
Alen Pamic

ZAGREB, Croatia

Hivi karibuni, Pamic alipoteza fahamu katika mechi ya ligi dhidi ya Lokomotiva iliyopigwa Februari, ambapo licha ya matatizo yake hayo alisisitiza kuendelea kucheza soka, huku madaktari wake wakimruhusu kufanya hivyo

NYOTA wa soka la kulipwa raia wa Croatia, Alen Pamic ameanguka uwanjani na kufariki dunia wakati wa mechi ndogo isiyo ya kimashindano, gazeti la kila siku la Vecernji List limesema katika toleo lake mtandaoni la leo Jumamosi.

Taarifa hiyo imeripotiwa kwa ufupi, huku ikiwa haina maelezo zaidi kuhusiana na kifo cha Pamic aliyekufa akiwa na umri wa miaka 23 tu.

Pamic, aliyekuwa akichezea klabu ya NK Istra 1961 katika ligi ya daraja la juu zaidi nchini hapa, alikuwa na historia ya matatizo ya moyo, ambayo yalimwangusha dimbani mara tatu kabla ya tukio hilo lililochukua uhai wake.

Hivi karibuni, Pamic alipoteza fahamu katika mechi ya ligi dhidi ya Lokomotiva iliyopigwa Februari, ambapo licha ya matatizo yake hayo alisisitiza kuendelea kucheza soka, huku madaktari wake wakimruhusu kufanya hivyo.

Pamic aliyekuwa kiungo mahiri dimbani, aliutumia msimu mmoja wa 2010/11 kuchezea klabu ya Standard Liege ya Ligi Kuu ya Ubelgiji, lakini klabu hiyo ikamtema muda mfupi baada ya kupata shambulio la moyo na kuzimia akiwa mazoezini, gazeti la Vecernji limesema katika taarifa yake.

Pamic ni mtoto wa nyota wa zamani wa kimataifa wa Croatia, Igor Pamic, ambaye kwa sasa anainoa klabu ya NK Istra 1961 aliyokuwa akiichezea marehemu.


Supersport.com

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*