
MEYA JERRY SILAA AWATAKA WATANZANIA KUTUNZA NA KULINDA AFYA ZAO ILI KUJENGA FAMILIA NA JAMII YENYE AFYA BORA.

Diwani
wa Kata ya Gongo la Mboto, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry
Silaa akipima Presha wakati wa kufunga zoezi la Utoaji wa Huduma za Afya
kwa Uwiano katika jamii ikiwa ni ishara ya kuhamasisha watu kujenga
utamaduni wa kupima Afya zao.
Wananchi wa Tanzania wameelezwa kuwa kazi ya kuboresha huduma za afya
na afya ya mazingira na maji ni ngumu na kuwa inahitaji nguvu za pamoja
kati ya jamii, halimashauri na wadau mbalimbali ili kupata mafanikio
yaliyokusudiwa hasa ya uzuiaji wa magonjwa.
Akitoa
nasaha wakati wa kufunga wa zoezi la utoaji wa huduma za afya kwa
uwiano katika jamii kata ya Gombo la Mboto, Mgeni rasmi Mh. Jerry Silaa,
Mstahiki Meya wa halmashauri ya Manispaa ya Ilala amesema huduma za
afya na afya ya mazingira ni muhimu katika maisha ya kila siku ya
binadamu.
Ameongeza
kwa kuwapongeza sana wakazi wa Gomngo la mboto Markaz pamoja na
viongozi wao kwa juhudi kubwa walioifanya katika kuhakikisha uwepo wa
kituo cha tiba karibu na jamii na kuwa wanastahili kuwa mfano wa kuigwa
na jamii zingine.
Aidha
amesema hilo ni moja wapo katika utekelezaji wa agizo la Mh. Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika lengo lake la kupeleka huduma za
tiba zikiwamo zile za zinazohitaji madaktari bingwa karibu na wananchi.
Pichani juu na chini ni wakazi wa Gongo la Mboto wakimsikiliza Diwani
wao ambaye pia ni Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Jerry Silaa
wakati wa kufunga zoezi la utoaji wa Huduma za Afya kwa Uwiano katika
Jamii kata ya Gongo la Mboto.


Comments