MKUTANO MKUU WA TFF SASA KUFANYIKA MWEZI UJAO KUJADILI MAREKEBISHO YA KATIBA
Rais wa Shirikisho la Mpira wa
Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga ametoa notisi kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu
Maalumu wa Shirikisho utakaofanyika Julai 13 mwaka huu kwenye ukumbi wa NSSF
Waterfront jijini Dar es Salaam ukiwa na ajenda moja ya marekebisho ya
Katiba.
Notisi hiyo imetolewa juzi
(Juni 12 mwaka huu). Rais ameitisha Mkutano huo kwa mujibu wa Ibara ya 25(1) ya
Katiba ya TFF baada ya kupata maagizo kutoka Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa
Miguu (FIFA) kwa barua yake ya Aprili 29 mwaka huu.
Ajenda rasmi na taarifa
nyingine zitatumwa kwa wajumbe siku 15 kabla ya Mkutano huo kwa mujibu wa Ibara
ya 25(4) ya Katiba ya TFF. Wanachama wa TFF ambao ni vyama vya mikoa, vyama
shiriki na klabu za Ligi Kuu wanatakiwa kutuma majina ya wajumbe
halali.
TFF inapenda kuwakumbusha
wanachama wake kutuma majina ya wajumbe halali ili kufanikisha maandalizi ya
Mkutano huo. Ni vizuri kuhakikisha kuwa jina linalotumwa ni la mjumbe halali wa
Mkutano Mkuu kwa mujibu wa Katiba ya TFF.
Comments