MNYAMA, YANGA NA SUPER FALCONS KAZI KWAO, ZARUHUSIWA KWENDA DARFUL!!
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamadauni na Michezo, Amos Makalla
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Siku chache baada ya Serikali ya Tanzania kukataa
kuziruhusu timu tatu za Tanzania, Simba , Yanga na Super Falcons ya visiwani
Zanzibar kushiriki michuano ya kombe la Kagame, leo hii Serikali imeziruhusu
klabu hizo kwenda Sudan kushiriki michuano ya Klabu Buingwa Afrika Mashariki na
Kati, Kombe la Kagame.
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Amos
Makalla akiongea na waandishi wa habari kanda ya kati Dodomo asubuhi ya leo
amesema wameruhusu klabu hizo ziende Sudan baada ya kuhakikishiwa na Serikali ya
nchi hiyo kwamba itatoa ulinzi wa kutosha dhidi ya timu za
Tanzania.
Makalla amesema wameandikiwa barua na Serikali ya
Sudan ikiwahakikishia kwamba timu za Tanzania zitapewa ulinzi mkubwa
zisiathirike na machafuko yanayoedelea Sudan.
Kufuatia tamko la Serikali kuziruhusu klabu hizo
sasa ziende Sudan, sasa ni juu yao ya klabu hizo kuamua kwenda au
kutokwenda.
Lakini Katibu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika
Mashariki na Kati (CECAFA), Mkenya Nicholas Musonye amekwishatishia
atazichukulia hatua kali klabu hizo zisipokwenda.
Juzi Serikali kupitia Makalla ilitoa tamko la
kuzuia klabu za Tanzania kutokwenda Sudan kutokana na machafuko yanayoendelea
nchini humo.
Kufuatia tamko hilo, jana Yanga, ambao ni
mabingwa watetezi kwa miaka miwili mfululizo, walitangaza kuvunja kambi yao hadi
wiki mbili baadaye, wakati Kombe la Kagame linaanza kutimua vumbi Juni 18, mwaka
huu.
Yanga wamepangwa Kundi C katika michuano hiyo
pamoja na Ports ya Djibouti, Express ya Uganda na Vital ‘O’ ya Burundi, wakati
wapinzani wao wa jadi, Simba SC wamepangwa Kundi A pamoja na wenyeji El-Mereikh,
Elman ya Somalia na APR ya Rwanda.
Katika michuano hiyo inayotarajiwa kufikia tamati
Julai 2, mwaka huu mjini Khartoum, Sudan, mabingwa wa Kenya, Tusker wamepangwa
Kundi B pamoja na wenyeji wengine, Al-Hilal, Falcons ya Zanzibar, Al Ahly Shandy
ya Sudan na Al-Nasir Juba ya Sudan Kusini.
Yanga wataanza kampeni zao za kutetea taji hilo
Juni 20 kwa kumenyana na Express, wakati Simba SC itashuka dimbani Juni 21
kufungua dimba na El-Mereikh, na mechi zote zitachezwa Elfashar
Comments