MWANDISHI TANZANIA DAIMA JAJI REDD'S MISS TANGA
Clezencia Tryphone |
Na Elizabeth John
MWANDISHI
wa Tanzania Daima Clezencia Tryphone ‘Tasha’ anatarajia kuwa jaji
katika shindano la kumsaka Redds Miss Tanga akisaidiana na aliyewahi
kuwa Miss Tanzania miaka kadhaa iliyopita.
Tasha,
anatarajia kufanya kazi pamoja na Miss huyo katika shindano hilo
linalotarajiwa kutimua vumbi Juni 22 katika uwanja wa Mkwakwani Mjini
humo.
Akizungumzia
uteuzi huu uliofanywa na Kampuni ya Datk ambao ni waratibu wa Shindano
hilo, Tasha alisema, amefarijika kupata nafasi hiyo ya kuwa jaji katika
shindano hilo na kuaidi kufanya kazi vema na Wema ili waweze kumpata
mrembo bora na mwenye vigezo.
Tasha
alisema, licha ya kuwa ni mara yake ya kwanza kuwa jaji wa shindano
hilo, amedai kuwa na uwezo na kazi hiyo kwa kuwa ni muumini mkubwa wa
mashindano mbalimbali ya umis hapa nchini.
“Kwanza
namshukuru mungu kwa uteuzi huu, naimani bila yeye mimi nisingepata
nafasi hiyo, na nimaimani nitafanya kazi vizuri kwa kushirikiana na
mwenzangu ili tuweze kumpata mrembo mwenye vigezo ambaye ataiwakilisha
vema Redds Miss Tanga na kutwaa taji la Taifa,”alisema Tasha.
Tasha
aliongeza kuwa mpaka sasa anaendelea na mafunzo ya ujaji ili aweze
kufanya kazi yake kwa ufasaha bila ya kuwepo kwa upendeleo dhidi ya mtu
yoyote.
Comments