NDOTO ZA USHINDI ZA MSAMBATAVANGU NA KINANA DHIDI YA KUKIGALAGAZA CHADEMA YATIMIA IRINGA
katibu mkuu wa CCM Bw Kinana akiagana na makada wa CCM mkoa wa Iringa hivi karibuni
Kada wa CCM mjini Iringa Bw Shukru Stivine akisalimiana na katibu mkuu wa CCM Taifa Bw Kinana leo mgombea udiwani wa CCM kata ya Mbalamaziwa wilayani Mufindi Bw Zuberi Nyomolela wa pili kushoto , wa kwanza kushoto ni mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Bi Jesca Msambatavangu na kutoka kulia wa kwanza ni katibu mwenezi na itikadi Taifa Nape Nnauye na katibu mkuu wa CCM Taifa Bw Kinana
Katibu mkuu wa CCM Taifa Bw Kinana akiwapongeza wanachama wa CCM kata ya Mbalamaziwa ambao walishindwa katika mchakato wa kura za maoni katika kinyang'anyiro cha udiwani ndani ya CCM kata hiyo
Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo katika kata ya Ng'ang'ange, msimamizi msaidizi wa uchaguzi huo, Esabela Kamwela alisema jumla ya wapiga kura 919 kati ya 1087 waliojiandikisha walishiriki uchaguzi huo.
Alisema Chadema ilimsimamisha Lucas Chahe huku CCM ikimsimamisha Nangamleki Yohanes katika uchaguzi huo uliomaliza katika hali ya utulivu na amani.
Katika kata ya Mbalamaziwa ambako ni jirani kabisa na kata ya Nyololo ambayo imeingia katika vitabu vya historia baada Septemba 2, mwaka jana wananchi wake kuhuhudia tukio ambalo halikuwahi kutokea katika nchi hii la mwandishi wa habari Daudi Mwangosi kuuawa wakati Chadema ikiendelea na harakati zake za kuimarisha chama chao, mgombea wake Ezekiel Mlyuka aliambulia kura 185 tu kati ya kura 1,611 zilizopigwa.
Mgombea wa CCM, Zuberi Nyomolelo aliibuka mshindi wa kiti
hicho cha udiwani baada ya kupata kura 1,426; kura 26 zikiharibika .
Katika mazingira ya kufurahisha, wagombea wa vyama vyote wameyakubali matokeo hayo, huku wafuasi wa CCM na wateule wao wakiendelea na shamrashamra wakisubiri siku ya kuapishwa kwa ajili ya kuwatumikia wananchi.
Kada wa CCM mjini Iringa Bw Shukru Stivine akisalimiana na katibu mkuu wa CCM Taifa Bw Kinana leo mgombea udiwani wa CCM kata ya Mbalamaziwa wilayani Mufindi Bw Zuberi Nyomolela wa pili kushoto , wa kwanza kushoto ni mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Bi Jesca Msambatavangu na kutoka kulia wa kwanza ni katibu mwenezi na itikadi Taifa Nape Nnauye na katibu mkuu wa CCM Taifa Bw Kinana
Diwani mteule wa kata ya Mbalamaziwa Mufindi aliyekisurubu vibaya Chadema Bw Zuberi
Nyomolela (kushoto) akiwana katibu mkuu wa CCM Taifa Bw Kinana hivi karibuni
wakati akimnadi katika kijiji cha Mbalamaziwa
Katibu mkuu wa CCM Taifa Bw Kinana akiwapongeza wanachama wa CCM kata ya Mbalamaziwa ambao walishindwa katika mchakato wa kura za maoni katika kinyang'anyiro cha udiwani ndani ya CCM kata hiyo
......................................................................................................................................
AHADI iliyotolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM)
mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu kwa katibu mkuu wa chama hicho Taifa,
Abdulaman Kinana kwamba watakibwaga
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika uchaguzi mdogo wa madiwani
mkoani hapa, imekuwa kweli.
Msambatavangu alimueleza Kinana alipopita hivi karibuni mjini
Iringa wakati akielekea mkoani Njombe kwa ziara ya kikazi kwamba CCM itapata
ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi huo katika kata ya Ng’ang’ange wilayani Kilolo na Mbalamaziwa, wilayani
Mufindi.
“Niliahidi na imekuwa kweli kwasababu kazi ya maendeleo inayofanywa
na serikali ya CCM inazidi kurejesha imani kwa wananchi na inadhihirisha jinsi
wanavyopuuza kelele za baadhi ya wanasiasa wanaopinga maendeleo yanayofanywa,”
alisema
Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo katika kata ya Ng'ang'ange, msimamizi msaidizi wa uchaguzi huo, Esabela Kamwela alisema jumla ya wapiga kura 919 kati ya 1087 waliojiandikisha walishiriki uchaguzi huo.
Alisema Chadema ilimsimamisha Lucas Chahe huku CCM ikimsimamisha Nangamleki Yohanes katika uchaguzi huo uliomaliza katika hali ya utulivu na amani.
Kamwela alisema katika uchaguzi huo kura 16 ziliharibika
huku mgombea wa Chadema akianguka
vibaya kwa kupata kura 217 na mgombea wa CCM akiibuka kidedea
kwa kuzoa kura 686.
Katika kata ya Mbalamaziwa ambako Chadema ilijipata matumaini ya ushindi kwa kile kilichoonekana mikutano yake kupata idadi kubwa ya watu, mgombea wake alibwagwa vibaya dhidi ya mgombea wa CCM.
Katika kata ya Mbalamaziwa ambako Chadema ilijipata matumaini ya ushindi kwa kile kilichoonekana mikutano yake kupata idadi kubwa ya watu, mgombea wake alibwagwa vibaya dhidi ya mgombea wa CCM.
Katika kata ya Mbalamaziwa ambako ni jirani kabisa na kata ya Nyololo ambayo imeingia katika vitabu vya historia baada Septemba 2, mwaka jana wananchi wake kuhuhudia tukio ambalo halikuwahi kutokea katika nchi hii la mwandishi wa habari Daudi Mwangosi kuuawa wakati Chadema ikiendelea na harakati zake za kuimarisha chama chao, mgombea wake Ezekiel Mlyuka aliambulia kura 185 tu kati ya kura 1,611 zilizopigwa.
Katika mazingira ya kufurahisha, wagombea wa vyama vyote wameyakubali matokeo hayo, huku wafuasi wa CCM na wateule wao wakiendelea na shamrashamra wakisubiri siku ya kuapishwa kwa ajili ya kuwatumikia wananchi.
Comments