REDD'S MISS MBEYA APATIKANA










HATIMAYE  Mkoa wa Mbeya umepata mwakilishi wa kushiriki kinyang’anyiro cha  Mrimbwende wa Redds Miss Tanzania baada ya shindano la kumpata  Miss Mbeya kukamilika.
Mratibu na Mwandaaji Miss Redds Mkoa wa Mbeya Gabriel Mbwile amesem jumla ya warembo 12 wameshiriki kinynganyiro hicho tangia wawekewe kambi hadi  siku ya shindano.
Ameongea kuwa mshindi wa kwanza amezawadiwa kitita cha fedha taslimu Milioni moja, mshindi  wa pili 750,000/=, mshindi wa tatu 500,000/= na wengine wote wamepewa  kifuta jasho cha  shilingi 100,000/=.
Amewataja washindi hao kuwa ni Jackline Luvanda mshindi wa kwanza, Aneth Brayton mshindi wa pili na Daina  Athlimani aliyeibuka msindi wa tatu.
Amewatja washiriki wengine kuwa ni Naba Magambo, Zainabu Matabi, Salma Abdalah, Flaviana Sixbert, Sarah Samwel, Aisha Beneka, Darlin Athani, Mwajabu Ngobai na Neema Raymond.
Aidha Mgeni rasmi katika kinyang’anyiro hicho  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya  Diwani Athumani, amezidi kusisitiza suala la amani kwa wakazi wa Mkoa wa Mbeya kwamba inapaswa kushughulikiwa ni kila mtu.

PICHA NA MBEYA YETU 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI