REDDS MISS SINZA 2013 FUNIKA MBAYA
Mkurugenzi wa Lino International Agency, Hashim “Uncle” Lundenga akisisitiza jambo na kwa warembo wa Redds Miss Sinza 2013 alipotembelea kambi ya mazoezi hayo. Warembo hao watapanda jukwaani Ijumaa kuwania taji la mwaka huu. (Picha/Mpiga picha wetu).
Na Mwandishi Wetu
.....................................................................................................................................................
Mkurugenzi wa kampuni ya Lino
International Agency, Hashim “Uncle” Lundenga amewafagilia warembo 12
wanaowania taji la Redds Miss Sinza 2013 kuwa kila mmoja anaweza kutwaa
taji hilo katika mashindano yaliyopangwa kufanyika kesho Ijumaa kwenye
ukumbi wa Meeda Club uliopo Sinza Mori.
Lundenga alisema hayo katika hotuba yake
fupi baada ya kutembelea kambi hiyo akiwa na kamati yake yote ya Redds
Miss Tanzania. Wajumbe wengine waliokuwepo katika msafara huo ni Bosco
“Mshua” Majaliwa ambaye ni Katibu Mkuu, Albert Makoye (Mkuu wa Itifaki),
Hidan Ricco (Afisa Uhusiano) na Yason Mashaka.
Alisema kuwa warembo wa Redds Miss Sinza
wanakazi kubwa ya kulinda heshima ya mwaka jana ambapo Brigitte Alfred
alitwaa taji hilona baadaye kutwaa taji la Miss Kinondoni na Tanzania.
“Mpo vizuri na ninatarajia kuona
ushindai mkubwa, naamini majaji watafanya kazi kubwa na mshindi
atakayepatikana atakuwa wa halali, kwani hakuna upendeleo katika
kutafuta mshindi, mara nyingi tumekuwa tukitafuta mrembo bora na si bora mrembo,” alisema Lundenga.
Alisema kuwa warembo wote 12 wanatakiwa
kujua uwa hakuna rushwa ya ngono katika mashindano hayo na wale
wanaosema hivyo wana lengo la kuharibu sifa ya mashindano hayo.
Aliongeza kuwa mshindano hayo yana miaka 20 sasa na washindi
wamepatikana kwa njia ya halali na kama kuna masuala ya ngon basi hiyo
ni tabia ya msichana na wala hayahusiani na mashindano.
Mratibu wa mashindano hayo, Majuto Omary
alisema kuwa maandalizi yamekamilika nay a Twanga Pepeta itatumbuiza
siku hiyo huku ikitambulisha baadhi ya nyimbo zake mpya zilizomo katika
albamu ya 12 ijulikanayo kwa jina la Nyumbani ni Nyumbani.
“Ikukmbukwe kuwa twanga pepeta haijatumbuiza Sinza kwa
kipindi kirefu na hivyo kuandaa zawadi
maalum kwa mashabiki wake katika mashindano hayo yaliyo dhaminiwa na
Redds Original, Dodoma Wine, Chilly Willy Energy Drink, Fredito
Entertainment, CXC Africa, Clouds Media Group, Salut5.com na Sufiani
Mafoto blog,” alisema Majuto.
Wakati huo huo, mbunifu wa mitindo,
Veronica Lugenzi atawavalisha nguo warembo hao watakaopanda jukwaani
kesho, Veronica ambaye alimvalisha nguo Miss Universe Tanzania wa mwaka
jana, amechukua jukumu hilo baada ya kuvutiwa na ubora wa warembo hao.
Mwisho…
Comments