STAR TV YAJITOA STAR TIMES

Na meneja Mipango na Utafiti wa Sahara Media Group Ltd, Nathan Lwehabura kwa niaba ya Uongozi, amewemgomea Nkoma wa TCRA;

Mei 23, 2013 Star Tv kupitia kwa mwanasheria wake iliwataka Star-Time kuiondoa kwenye king’amuzi chao ifikapo saa 6:00 Usiku Mei 31, mwaka huu kutokana na kurusha na kuuza maudhui ya vipindi vyake bila idhini na kukiuka sheria na haki za Hakimiliki.
Katika barua hiyo Star Tv iliwakumbusha Star-Time hawakuwa na mkataba wa kurussha vipindi vya kituo hicho kwa mujibu wa sheria ya Mawasiliano ya EPOCA na pia hawana haki ya kutumia maudhui ya yake bila idhini yao chi ni ya sheria ya hakimiliki ya Tanzania na Kimataifa.
Mei 31 mwaka huu, Star-Time (Star Media) walijibu kwamba hawajakiuka sheria yoyote na kusisitiza kwamba wataendelea kurusha matangazo hayo kutekeleza matakwa ya Sheria ya EPOCA na sheria zake, na Juni 6 mwaka huu Star TV iliwaandikia tena Star-Time na kusisitiza nia yake ya kuchukua hatua zaidi kutokana na kuendelea kukaidi ombi hilo la kusitisha matangazo hayo na kuainisha mapungufu kadhaa ya kisheia kwa upande wao yanayoifanya Star Tv ijiondoe katika king’amuzi chao ifikapo Juni 8 mwaka huu.
Star Tv ilieleza Star Media inayomilikiwa kwa pamoja na TBC na Star-Time kwamba inayo leseni ya miondo mbinu ya kurusha matangazo ya Televishane ya kupitia mafumo wa (Multiplex Operator License DTT) inayowaruhusu kuingia makubaliano ya Huduma na vituo mbalimbali kuwarushiwa matangazo yao, lakini Star –Time hawana leseni ya kutoa huduma ya mahudhui ambayo ni Content Service Provider License.
Star-Time ni kampuni ya kimataifa iliyoanzishwa China inayotoa huduma za mahudhui katika nchi mbalimbali za afrika ikiwamo Tanzania ili kupata mahudhui inalazimika kuingia mktaba na vituo vya Televisheni kabla ya kuviingiza kwenye King’amuzi chake na baadaye kuuza mahudhui hayo kwa walaji kwenye Mataifa hayo.
Star-Time inachukua vituo vya Televisheni bila idhini yao na kuweka katika King’amuzi chake kwa kisingizio kamba wanaruhusiwa na sheria ya EPOCA na kanuni zake, lakini sheria hiyo inasisitiza kuwapo kwa mkataba wa makubaliano (SLA) kwa pande zote husika.
Kwa mujibu wa mahudhi ya TV za Tanzania yanauzwa kwa walaji katika nchi nyingine kama Rwanda, Kenya, Uganda, Burundi na Nigeria bila idhini ya wamiliki wake na kwamba wanaomiliki mahudhui hazina uwezo wa kuidhibiti Star Time isirushe mahudhui yao nje ya nchi ya Tanzania kwa kuwa baadhi ya mahudhui wanayonunua nje kama Tamthilia na vipindi vinginevyo haviruhusiwi na watunzi au wasambazi wake kurushwa nje ya nchi.
Lakini uhusiani wa makampuni haya mawili ya Star Media (T) na Star-Time ya China yenye matawi mengi nchini Afrika katika uendeshaji wa matangazo ya Dijitali haijabainisha vizuri ili kujua nani ni nani na nini anachofanya hapa Tanzania katika misingi ya maelewano ya biashara, hivyo kutokana na mantiki ya hoja hizo Star –Time waliiondoa mara moja Star TV kwenye King’amuzi chao kama walivyoeolekewa na Star TV hiyo Juni 8.
Star Tv haioni sababu za kulazimishwa na TCRA kurushwa na Star Time pasipo kuondoa hitilafu hizo za kisheria na bila kuangalia sheria nyingine zinazolinda haki za TV huru kama sheria ya Hakimiliki na sheria za Ushindani katika soko moja. TCRA kwa kutozingatia hili inataka kujifanya mmiliki wa sheria hata zisizokuwa chini ya mamlaka yao..

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.