THE
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512,
2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
Fax: 255-22-2113425 |
|
PRESIDENT’S OFFICE,
THE
STATE HOUSE,
P.O. BOX
9120,
DAR
ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Ndugu
Wahariri, tunapenda kuwataarifu kuwa mwili wa Marehemu Mzee Timothy Apiyo (Katibu
Mkuu Kiongozi Mstaafu), aliyefariki siku ya Jumatatu 10, Juni 2013 katika
Hospitali ya Millpark, Johannesburg, Afrika Kusini,
utawasili katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere – DSM kesho, Ijumaa
14 Juni, 2013 saa moja usiku. Baada ya kupokelewa mwili utapelekwa nyumbani
kwake Ukonga Sitakishari ambako mwili utalala hapo.
Shughuli
za kuaga mwili wa Marehemu Mzee Timothy Apiyo zitafanyika siku ya Jumamosi 15,
Juni 2013 katika viwanja vya KARIMJEE kuanzia saa 2.00 asubuhi hadi saa 4.00
asubuhi.
Baada
ya hapo mwili wa marehemu Mzee Timothy Apiyo utapelekwa uwanja wa ndege wa Mwalimu
Julius Nyerere tayari kwa safari ya kwenda Rorya kwa ajili ya mazishi.
Tunaomba
ushirikiano wenu.
“ASANTENI”
Imetolewa na:
Kurugenzi
ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar
es Salaam.
13 Juni, 2013
Comments