Skip to main content

VITENDO VYA UJANGILI KATIKA HIFADHI VIPIGWE VITA , POLISI RUVUMA WAKAMATA MENO 18 YA TEMBO

 

Kamanda wa Polisi mkoani Ruvuma  Deusdedit Nsimeki akipanga maneno ya tembo kulingana na uneno /uzito kabla ya kuzungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.
 Mwandishi wa habari wa  Gazeti la Mtanzania Hamoni Mtega akiwa amenyanyua jino la tembo
-------------------------------------------------- 
JESHI  la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kukamata meno ya Tembo  18 yenye uzito wa kilo 84 yenye  thamani ya Tsh216,000,000/ambapo meno hayo 18 ni sawa na dola 15 elfu za kimarekani pia ni sawa na Tembo tisa waliouwawa .
 Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake leo Kamanda wa polisi mkoani Ruvuma  Deusdedit Nsimeki amesema kuwa tukio hilo la kukamata meno hayo lilitokea Juni 20 Mwaka huu majira ya saa 3.00 usiku  katika kijiji cha Majala kata ya Nandembo iliyopo wilaya  ya Tunduru mkoani Ruvuma .
 Kamanda Nsimeki amesema kuwa  tukio hilo la kukamatwa kwa meno hayo ya tembo lilitokea  baada ya askari polisi wa wilaya hiyo kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema ndipo wao waliweka mtego wa kuwanasa watuhumiwa hao lakini bahati mbaya watuhumiwa hao walikurupuka na kuacha mizigo ya meno hayo iliyokuwa imefungwa kwenye mifuko tofauti tofauti.
  Alisema kuwa watuhumiwa waliokurupuka walikuwa wanne huku kila mmoja na baiskeli ambazo walikuwa wamebebea meno hayo na kwa upande wa watuhumiwa wa meno ya tembo kukurupuka bila kutiwa mbaroni na jeshi hilo limekuwa ni tukio la pili la kwanza  lilitokea katika  kijiji  cha Hanga wilayani Namtumbo na la pili ndiyo hilo la wilaya ya Tunduru zote za mkoani Ruvuma .
 Aidha kamanda alisema kuwa jeshi la polisi linajitahidi kuwasaka watu ambao wamejificha na wanajihusha na matukio hayo ya ujangili kwa wanyama  na hasa tembo.
            
Pia ametoa wito kwa wananchi uendelea kushirikiana jeshi la polisi mkoani Ruvuma kwa kutoa taarifa za siri zitakazowezesha kukamatwa kwa wahusika wa vitendo vya uhalifu wa aina yoyote kwa sababu suala la ulinzi ni kila mmoja hivyo kunasoaswa kuwepo kwa ushirikiano wa karibu baina ya polisi na wananchi.na  Demashonews Blog 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.