WANAHABARI NCHINI WATAKIWA KUSHIRIKIANA NA JESHI LA MAGEREZA

Kamishina Jenerali wa Magereza CGP John C. Minja wa kwanza kutoka kulia, akizungumza na viongozi wa Tone Multimedia Group ambao ni wamiliki wa Mtandao wa Mbeya yetu Blog, Kushoto  ni Joseph Mwaisango, Fredy njeje na Venance Matinya kutoka Gazeti la Jambo leo  na Ezekiel Kamanga ambaye alikuwa amepiga Picha.
 Kamishna wa wa Magereza Gaston Sanga (Aliye vaa Tai) ambaye pia  Mkuu wa kitengo cha Fedha na Utawala wa Jeshi Hilo,akiwa sambamba na afisa Habari wa Jeshi la Magereza Mkaguzi Lukas A.Mboje wa pili kutoka kulia , Akizungumza na waandishi wa Habari.
 Kamishina Jenerali wa Magereza CGP John C. Minja kutoka kulia akizunguza na SACP C. A Keenja
 Kamishina Jenerali wa Magereza CGP John C. Minja kutoka kushoto akiwa na Mkuu wa uhamiaji Mkoa wa Mbeya Wilson Bambaganya.
 Mkuu wa kitengo cha Usafirishaji Makao makuu Jeshi la Magereza (wapili kutoka Kulia) Mratibu Mwandamizi wa Magereza Lazaro Nyanga akiwa na Afisa Habari wa Jeshi la Magereza pamoja na waandishi wa Habari
Kamishina Jenerali wa Magereza CGP John C. Minja katikati  akiwa katika na picha ya pamoja na Kamishna wa wa Magereza Gaston (kushoto) ambaye pia  Mkuu wa kitengo cha Fedha na Utawala wa Jeshi na Mkuu wa uhamiaji Mkoa wa Mbeya Wilson Bambaganya (kulia)
Kamishina Jenerali wa Magereza CGP John C. Minja akizungumza na baadhi ya Askari wa Jeshi la Magereza .
JESHI  la Magereza Nchini limeomba ushirikiano na Vyombo vya Habari ili kusaidia kufikia malengo ya kulisaidia Jeshi hilo kujitegemea  na kujiendesha lenyewe pasipo kutegemea misaada.
Kauli hiyo imetolewa na Kamishina Jenerali wa Magereza Nchini, CGP John C. Minja wakati wa hafla fupi ya kuwatunuku Nishani Maaskari wa Jeshi hilo iliyofanyika katika ukumbi wa Gereza la  Ruanda Jijini Mbeya alipokuwa akizungumza na baadhi ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya wakiwemo viongozi Waandamizi wa Mtandao wa www.mbeyayetu.blogspot.com.
Minja amesema ili kufikia malengo waliyojiwekea ni lazima pawepo na ushirikiano baina ya Jeshi hilo na Waandishi wa Habari kwa kuwa ndiyo wenye dhamana ya kuwaambia wananchi Changamoto zinazolikumba Jeshi hilo.
Pia ametoa wito kwa Viongozi kutoogopa kuzungumza na Vyombo vya Habari kwa kile alichodai kushindwa kufanya hivyo ni  kuficha maovu ambayo wanaogopa kuonwa na kujulikana kwa jamii.
Aidha amewaagiza Viongozi wa Jeshi hilo kuhakikisha wanaandaa Barua mapema kwa Maaskari wanaopandishwa Vyeo na siyo kusubiri na kusotea kwa muda mrefu wakisubiri barua za uthibitisho.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI