WAWILI WAKAMATWA KUFUATIA TUKIO LA KUVAMIWA MBUNGE WA KASULU


ACP-David Misime
Mnamo tarehe 20/06/2013 majira ya 19.00 hrs maeneo ya Area ‘E’ Manispaa ya Dodoma Mheshimiwa MOSES S/O MACHALI, miaka 31, Muha, Mbunge wa Kasulu Mjini kupitia NCCR – Mageuzi wakati anaelekea nyumbani kwake anakoishi njiani alikutana na vijana wanne (4) walikouwa amesimama katikati ya barabara akapiga honi lakini hawakupisha. Aliamua kuwauliza “Jamani mnasimama katikati ya barabara si nitawagonga?” 
Nao wakamjibu: “Wewe si unajifanya motto wa Mbunge, tutakupiga sasa”.

Alipojaribu kupita walipiga gari lake. Ilimbidi ashuke ili atazame kama gari hilo limepata uharibifu. Ndipo vijana hao wakaanza kumshambulia kwa ngumi na mateke huku naye akijitahidi kujihami, ndipo wakatokea vijana wawili (2) na kumsaidia. Kijana mmoja kati ya waliokuwa wanamshambulia Mheshimiwa Machali ‘alimng’ata’ mgongoni kijana aliyekuwa anamsaidia Mheshimiwa Mbunge.

Watuhumiwa baada ya kuona wamezidiwa nguvu walitimua mbio. Mheshimiwa Machali aligundua kuwa simu yake ya mkononi wameondoka nayo.
Msako mkali ulifanyika na usiku wa manane watuhumiwa wawili (2) walikamatwa ambao ni:-

1.         JEREMIA S/O LAWRENT MKUDE@ JERRY, Miaka 18, Mkaguru, Mkulima, Mkazi wa Chaduru, Manispaa ya Dodoma. Huyu amekutwa akiwa na jeraha usoni alilopata wakati anapambana na Mheshimiwa Mbunge na vijana waliokuwa wanamsaidia.
2.         CHARLES S/O CHIKUMBILI, Miaka 22, Mkulima, Mkazi wa Swaswa, Manispaa ya Dodoma.
Watuhumiwa walipokamatwa usiku huo wa manane wamekutwa na misokoto miwili (2) ya bhangi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU