Waziri wa Nishati na Madini akutana na Rais wa Kampuni ya Chiyoda Corporation ya Japan


Waziri wa Nishati na Madini, Mh.Profesa Sospeter M. Muhongo, akimfafanulia jambo Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Chiyoda Corporation ya Japan, Bw. Shogo Shibuya. Waziri Muhongo alikutana na Bw. Shogo kwa lengo la kufanya mazungumzo kuhusu uwekezaji nchini kwenye miradi ya uzalishaji wa umeme kwa kutumia jua pamoja na ujenzi wa miundombinu ya usindikaji wa gesi asilia na mitambo ya kuzalisha umeme. Mkutano huo ulifanyika mjini Yokohama, Japan wakati wa Mkutano wa tano wa Kimataifa wa Tokyo unaojadili Maendeleo ya Afrika (Tokyo International Conference on African Development (TICAD V) uliohudhuriwa na Wakuu wa nchi za Afrika na Japan pamoja na Mawaziri na Maofisa wa Serikali hizo. Mkutano ulifanyika tarehe 1 hadi 3 Juni, 2013.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.