Meneja wa
Kituo cha redio ya Jamii FADECO, Adelina Lwedamula (kushoto), akitoa
maelezo machache ya utengenezaji wa vipindi kwa Meneja Mahusiano ya
Jamii wa Airtel Tanzania Hawa Bayumi alipotembelea Studio za Redio hiyo
inayorusha matangazo yake kwenye mnara wa Airtel ambapo itawezesha
kupanua wigo wa matangazo yao kwa jamii.
**********************************
.Zaidi ya watu milioni mbili sasa kufikiwa na mawasiliano ya Radio FADECO kufuatia uzinduzi huo.
Airtel
Tanzania kwa kushirikiana na lisilo la kiserikali la United Nations
Educational, Scientific and Cultural Organization (UNESCO) wamezindua
mradi wa kuwawezesha radio za kijamii kwa kuwapatia vifaa vya radio na
kuwaunganisha na mitambo ya mawasiliano ili kuwafikia wananchi wa
pembezoni kwa urahisi zaidi.
Airtel na UNESCO) kupitia mradi
huo watawawezesha wananchi wa pembezoni kupata taarifa na matangazo
mbalimbali ya kijamii, kiutamanduni , Kiuchumi na kupata elimu juu ya
maswala mbalimbali ya kijamii.
Mradi huo wa kipekee ulizinduliwa
rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali Mstaafu Fabian Masawe ambae
aliwatia moyo Airtel na UNESCO kuendelea na moyo huo wa kusaidia jamii
kupitia radio zao za kijamii ambazo ndio zipo karibu na wananchi wa
vijijini. Aidha aliwataka wananchi wa Karagwe kuitumia radio hii kwa
maendeleo ya jamii na kuendeleza shughuli zao za kiuchumi.
Akizungumza
na Waandishi wa Habari katika uzinduzi rasmi wa mradi katika radio ya
FADECO Karagwe, Meneja Mahusiano ya Kijamii, Hawa Bayumi alisema kwamba
mradi huo kwa kushirikiana na UNESCO utawanufaisha watu wa pembezoni
ambao radio za kijammii (Community Radios) ndio kimbilio lao la karibu
katika kupata habari na taarifa mbalimbali.
Alisema radio za
kijamii ni radio za kipekee ambazo zinawafikia kwa urahisi watu wa
pembezoni katika kupata taarifa za elimu ya jamii, Afya, uchumi,
ujasirimali na stadi za maisha ili kuwawezesha wananchi kujikwamua
kiuchumi. Radio za kijamii zina uwezo wa kuwafikia wananchi kwa haraka
zaidi na radio hizo zipo karibu na wananchi aliongeza Bayumi
“kwa
upande wake Afisa mradi wa habari na mawasiliano UNESCO Yusuph Al
Aminalisema tupo na ushirikiano na radio za jamii kama nane na leo
tumeanza na radio ya Fadeco . maendo mengine yatakayonufaika na mradi
huu ni pamoja na Sengerema Mwanza, Chake Chake Pemba, Makunduchi Unguja
, Pangani Tanga, Kyela Mbeya , Kahama Shinyanga, Loliondo Arusha na
Uvinza Kigoma.
Al Amin alisema radio za jamii ni muhimu katika
kuelimisha wakinamama na maswala ya ujasirimali, uzazi wa mpango na ni
wadau muhimu katika kuleta maendeleo kwenye jamii husika. radio za
kijamii ni mdau mkubwa wa kuwawezesha na kuwafundisha wananchi umuhimu
wa kufanya kazi ili kujikwamua kiuchumi.
Kwa upande wake
Mkurugenzi wa radio FADECO bwana Joseph Sekiku alisema tunawashukuru
sana Airtel na UNESCO kwa kuboresha ufanisi wa huduma zetu za radio hapa
Karagwe , sasa radio yetu inaweza kusikika kwa usikivu zaidi katika
maeneo mbalimbali ya Wilaya karagwe na wilaya za jirani kama vile
Wilaya ya Kyirwa, Wilaya Missenyi, wilaya ya Bukoba vijijini na mjini,
wilaya ya Muleba, Biharamuro na Ngara , hii ni takribani watu wapatao
zaidi ya milioni 2 sasa wanapata mawasiliano ya radio tofauti na
ilivyokuwa awali. Kwa kweli haya ni mafanikio makubwa na tunawashukuru
sana kwa hilo.
Kupitia mradi huo kampuni ya Airtel imeweza
kuwapatia modem na simcard radio za kijamii ili kuwawezesha waandishi
wao wa Habari kufanya kazi kwa ufanisi.
Mradi wa Radio ni program
maalum inayoendeshwa na Airtel kwa kushirikiana na UNESCO yenye lengo
la kusaidia jamii zilizo na changamoto mbalimbali ikiwemo za mila
potofu, elimu duni, ukeketwaji, imani za kishirikina, maendeleo duni ,
ukandamizaji wa wanawake na watoto na changamoto nyingi zinginezo. Lengo
hasa ni kuinua mawasiliano katika maeneo ya vijiini nchini.
|
Comments