ARSENAL YAENDELEZA MAUWAJI, YAWAFUMUA 7-1 WAVIETNAM LEO

IMEWEKWA JULAI 17, 2013 SAA 5:00 USIKU
ARSENAL imeendeleza wimbi la ushindi mnono katika mechi za kujiandaa na msimu, baada ya leo kuifumua mabao 7-1 Vietnam XI kwenye Uwanja wa My Dinh mjini Hanoi.
Ushindi huo umemoa majibu kadhaa kocha Arsene Wenger, kwanza kama atashindwa kusajili mshambuliaji wa kiwango cha dunia kabla ya mechi ya ufunguzi ya Ligi Kuu England dhidi ya Aston Villa, Olivier Giroud atatosha kwenye kampeni ya ushindi baada ya leo kufunga mabao matatu peke yake.
Pili, anaweza kumtumia Bacary Sagna katika beki ya kati itakapotokea dharula kama atakwama kumsajili beki wa Swansea, Ashley Williams baada ya beki huyo kulia wa Arsenal kucheza namba nzuri leo.
Na tatu, inayoweza kuwa muhimu kuliko zote, Jack Wilshere na kama yuko fiti kabisa kuanza msimu, baada ya kucheza mechi yake ya kwanza leo tangu afanyiwe upasuaji wa kifundo cha mguu Mei.
Thanks! The Arsenal players carry a 'Thank You' banner and wave to fans after defeating Vietnam
Shukrani! Wachezaji wa Arsenal wakiwa wamebeba bango la 'Asanteni' kwa ajili ya mashabiki baada ya kuwafunga Vietnam
Challenge: Arsenal's Bacary Sagna tackles Vietnam's Nguyen Anh Duc
Shughuli: Beki wa Arsenal, Bacary Sagna akiupitia mpira miguuni mwa Nguyen Anh Duc wa Vietnam

Mbali na mabao matatu ya Giroud, mabao mengine ya Arsenal leo yamefungwa na Alex Oxlade-Chamberlain, Chuba Akpom mawili na Ignasi Miquel ambao wote walifunga pia kwenye ushindi wa 7-0 katika mchezo wa kwanza dhidi ya Dream Team ya Indonesia.
Kikosi cha Arsenal leo kilikuwa; Szczesny/Martinez dk71, Sagna/Aneke dk71, Jenkinson/Olsson dk71, Koscielny/Mertesacker dk46, Gibbs/Miquel dk46, Arteta (Nahodha)/Ramsey dk46, Rosicky/Zelalem dk46, Oxlade-Chamberlain/Wilshere dk66, Gnabry/Walcott dk46, Podolski/Miyaichi dk46 na Giroud/Akpom dk46
Watching it fly in: Olivier Giroud scores one of his goals against Vietnam
Olivier Giroud akifunga moja ya mabao yake leo
Put it there: Chuba Akpom celebrates his goal with his teammate Alex Oxlade-Chamberlain
Chuba Akpom akishangilia bao lake na mchezaji mwenzake, Alex Oxlade-Chamberlain
Break through: Giroud strides past his opponent during a very straightforward victory for Arsenal
Giroud akifanya safari
Chuba Akpom
Chuba Akpom
Chuba Akpom akishangilia bao lake leo
Serge surge: Serge Gnabry takes on the Vietnam defence
Serge Gnabry akipasua ngome ya Vietnam
Speedster: Alex Oxlade-Chamberlain was also on target during the 7-1 win
Alex Oxlade-Chamberlain pia alifunga leo
Battle: Vietnam's Pham Thanh Luong vies for the ball with Arsenal's Bacary Sagna

RATIBA YA MECHI ZA ARSENAL KUJIANDAA NA MSIMU

Julai 14 na Indonesia XI walishinda 7-0
Julai 17 na Vietnam wameshinda 7-1
Julai 22 na Nagoya Grampus (Uwanja wa Toyota, Japan) Saa 5.30 asubuhi
Julai 26 na Urawa Red Diamonds (Uwanja wa Saitama, Japan - Kombe la Saitama City) Saa 5.30 asubuhi
Agosti 3 na Napoli (Kombe la Emirates) Saa 10.20 jioni
Agosti 4 na Galatasaray (Kombe la Emirates) Saa 10.20 jioni
Agosti 10 na Manchester City (Uwanja wa Olimpiki, Helsinki) Saa 9 jioni

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*