BALOZI MULAMULA AWASILI WASHINGTON, DC KUANZA MZIGO

Balozi Liberata Mulamula akishuka kwenye gari Bethesda, Maryland wakati akitokea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Dulles uliopo Sterling, Virginia Ijumaa July 12, 2013. Mhe, Mulamula ndiye Balozi wa Tanzania nchini Marekani aliyekuja kuchukua nafasi ya Balozi Mwanaidi Maajar aliyemaliza muda wake mwanzoni mwa mwaka huu. Kabla ya hapo Balozi Mulamula alikua Balozi wa maziwa makuu na msaidizi wa Rais mwandamizi katika maswala ya diplomasia.

Mhe. Liberata Mulamula akisalimiana na Maafisa na Wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani waliofika kumlaki kwenye yatakayokua makazi yake Bethesda, Maryland.

 Mhe. Liberata Mulamula akisalimiana na Maafisa na Wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani waliofika kumlaki kwenye yatakayokua makazi yake Bethesda, Maryland.
Balozi Liberata Mulamula akisalimiana na Maafisa na Wafanyakazi wa Ubalozi (hawapo pichani) wakati walipomkaribisha nyumbani kwake, Bethesda, Maryland.
Watoto wa Mhe. Balozi Alvin na Tanya.
 Mume wa Mhe. Balozi, Bwn. George Mulamula.
Kaimu Balozi na mkuu wa Utawala na Fedha, Mama Lily Munanka katika picha.

Mhe. Balozi Liberata Mulamula akibadlishana mawili matatu na Maafisa na Wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani wakati walipomkaribisha nyumbani kwake Bethesda, Maryland kushoto ni Afisa Ubalozi Mindi Kasiga.

 Juu na chini ni Maafisa na Wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani wakiwa tayari kumpokea Mhe. Balozi Mulamula na familia yake.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.