Brotherhood kuendelea na maandamano


Wafuasi wa Brotherhood
Kundi la Muslim Brotherhood limeapa kuendelea na maandamano ya amani kupinga kuondolewa madarakani kwa Rais Mohammed Morsi na jeshi la nchi. Wafuasi wa Mosri wamekua wakiandamana mjini Cairo karibu na kambi kuu ya jeshi anakoaminika amezuiliwa.

Taarifa ya Brotherhood inajiri wakati kumetolewa kibali kuwakamata viongozi wake wakuu. Hapo Jumatatu wiki hii wafuasi wa kundi hilo zaidi ya 50 waliuawa katika makabiliano na jeshi.
Huku haya yakiarifiwa Marekani imetangaza kwamba itatoa ndege za kivita aina ya F-16 kwa jeshi la Misri katika majuma yajayo. Utawala wa Rais Barack Obama inaendelea kutafakari matukio yaliyotokea Misri wiki jana.
Ufadhili wa jeshi ungesitishwa mara moja endapo mwingilio huo wa jeshi ungelionekana kuwa mapinduzi. Hapo Jumatano maafisa wa Misri walitoa kibali cha kukamatwa viongozi wa Muslim Brotherhood akiwemo kiongozi mkuu Mohammed Badie.
Viongozi hao wamelaumiwa kwa kuchochea ghasia ambapo wafuasi wao waliuawa pamoja na maafisa watatu wa usalama. Tayari ratiba ya uchaguzi mpya imetangazwa na Rais mpya anatarajiwa kuchaguliwa mwakani sawa na bunge.
Katiba itafanyiwa marekebisho na kupigiwa kura ya maoni kabla ya mwisho wa mwaka huu.Kundi la Brotherhood limepinga mpango mpya na kuapa halitashiriki mchakato wowote bila Mohammed Morsi kurejeshwa madarakani.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA